Friday, October 26, 2012

TFDA NYANDA ZA JUU KUSINI KUDHIBITI VIPODOZI


MAMLAKA ya chakula na dawa (TFDA) kanda ya Nyanda za juu kusini mkoani Mbeya imeweka mikakati ya kudhibiti vipodozi feki vinavyopitishwa katika mipaka isiyo rasmi kinyume cha sheria.


Kaimu Meneja wa mamlaka hiyo Pual Sonda amesema hayo jana ofisini kwake alipokuwa akizungumza na Mtandao weu kwa kuwataka watumiaji na wafanyabiashara hiyo kuacha kwani wamejipanga vilivyo kukabilina na biashara hiyo haramu.


Amesema kuwa wanazidi kuimarisha ulinzi katika mipaka ilio rasmi inayozunguka mkoa huu ambayo ni Kasumulo na Tunduma ingawa kuna mipaka isiyo rasmi inayotumiwa kupitisha vipodozi hivyo.


Ameongeza kuwa vipodozi hivyo vina madhara kwa watumiaji husababisha magonjwa kama uzio wa ngozi, kanda ya ngozi, uzio wa ubongo na kupoteza fahamu na maisha hivyo kupunguza nguvu kazi za taifa.


Alimesema kuwepo kwa usambazaji wa dawa feki za kupunguza makali ya Ukimwi (ARV) sonda amesema wamejipanga kukabiliana nalo kwa kukagua bohari ya dawa (MSD), hospitalini na viwandani na kugundua kuwa dawa hizo feki hazipo.


Pia amesema wanatoa elimu juu ya vipodozi feki kupitia vyombo vya habari, vipeperushi hata maonesho mbalimbali ya kitaifa hivyo wananchi watoe ushirikiano kwa kupiga simu katika mamlaka hiyo kwani mawasiliani wameshayatoa.


“Tunatoa elimu kupitia vyombo vya habari na katiba maonesho mbalimbali ya kitaifa hivyo wananchi wabadilike kwani vipodozi hivyo vina madhara makubwa”alisema Sonda.


No comments:

Post a Comment