Monday, May 14, 2012

MTWANGA INJILI WA MIAKA 46 ABAKA KIBINTI CHA MIAKA 14

  OBED Mwakilasa (46), mkazi wa Kijiji cha Mwela, Kata ya Kandete wilayani Rungwe mkoa wa Mbeya ametuhumiwa kumbaka mtoto wa kike mwenye umri wa miaka 14 na kumsababishia maumivu makali katika mwili wake.

Mwenyekiti wa Kijiji hicho Bw. Anania Mwalukasa amesema tukio hilo limetokea Mei 10 mwaka huu, ambapo mtuhumiwa anadaiwa alimuita mtoto huyo kwenye shamba la michai kisha kumfanyia ukatili huo.

Baada ya kukuta anakumbana na mkono wa sheria Mwalikasa alienda kuomba msamaha kwa wazazi wa mtoto huyo ili wamsamehe, ombi ambalo lilipokelewa na kusamehewa.

Aidha imedaiwa kuwa mtuhumiwa huyo alifika kijijini hapo kwa mbinu ya kuhubiri neno la Mungu.

Kwa upande wake Mwenyekiti Bwana Mwalukasa ameonekana kukasirishwa na kitendo cha wazazi hao kusameheana nyumbani na kudai kuwa tabia hiyo ikiendekezwa itasababisha kuendelea kwa vitendo viovu kijijini hapo.

Madhara hayo yaliyosababishwa na Bw. Mwakilasa kwa mtoto huyo hayajaweza kufahamika kutokana na wazazi kutompeleka mtoto wao kufanyiwa uchunguzi katika Kituo chochote cha huduma ya Afya(Zahanati/Kituo cha afya/Hospitali).

Hata hivyo vitendo hivyo vya ubakaji wilayani humo vimeota mizizi kutokana na baadhi ya wazazi kufumbia macho kwa kupewa pesa.

No comments:

Post a Comment