OBED Mwakilasa (46),
mkazi wa Kijiji cha Mwela, Kata ya Kandete wilayani Rungwe mkoa wa Mbeya ametuhumiwa
kumbaka mtoto wa kike mwenye umri wa miaka 14 na kumsababishia maumivu
makali katika mwili wake.
Mwenyekiti wa Kijiji hicho Bw.
Anania Mwalukasa amesema tukio hilo limetokea Mei 10 mwaka huu, ambapo
mtuhumiwa anadaiwa alimuita mtoto huyo kwenye shamba la michai kisha
kumfanyia ukatili huo.
Baada ya kukuta anakumbana na mkono
wa sheria Mwalikasa alienda kuomba msamaha kwa wazazi wa mtoto huyo ili
wamsamehe, ombi ambalo lilipokelewa na kusamehewa.
Aidha imedaiwa kuwa mtuhumiwa huyo alifika kijijini hapo kwa mbinu ya kuhubiri neno la Mungu.
Kwa upande wake Mwenyekiti Bwana
Mwalukasa ameonekana kukasirishwa na kitendo cha wazazi hao kusameheana
nyumbani na kudai kuwa tabia hiyo ikiendekezwa itasababisha kuendelea
kwa vitendo viovu kijijini hapo.
Madhara hayo yaliyosababishwa na
Bw. Mwakilasa kwa mtoto huyo hayajaweza kufahamika kutokana na wazazi
kutompeleka mtoto wao kufanyiwa uchunguzi katika Kituo chochote cha
huduma ya Afya(Zahanati/Kituo cha afya/Hospitali).
Hata hivyo vitendo hivyo vya ubakaji wilayani humo vimeota mizizi kutokana na baadhi ya wazazi kufumbia macho kwa kupewa pesa.
No comments:
Post a Comment