Wednesday, May 8, 2013

FRANCIS CHEKA APONGEZWA NA IBF




http://www.gushit.com/files/bookmark_photos/abcffd70f4L.jpgShirikisho la Ngumi la Kimataifa (IBF) limempongeza bondia wa kitanzania, Francis Cheka kutokana na uwezo mkubwa alionao kwenye ndondi katika uzito Super Middle wa viwango vya kimataifa.
 Cheka alifanikiwa kutetea mkanda wake wa IBF Africa katika uzito huo baada ya kumshinda kwa KO bondia Thomas Mashali a.k.a “Simba asiyefugika” Mei Mosi mwaka 2013 katika ukumbi wa PTA jijini Dar Es Salaam.
IBF imefikia hatua ya kumpongeza mwanamasumbwi huyo baada ya ushindi huo ambao umedhihirisha kuwa yeye  ni bingwa wa bara la Afrika na anatazamiwa kurudiana na bondia wa Malawi Chimwemwe Chiotcha mnamo Agosti katika mpambano la kutetea mkanda wake.
Mpambano huo wa marudiano utafanyika katika jiji la Blantyre nchini Malawi na tayari majadiliano ya  yanaendelea vizuri na Kampuni ya “Mawenzi Boxing Promotion” ya nchini Malawi ikisimamiwa na Stephen Mawezni ndiyoitakayoandaa mpambano huo. 
Pambano hili linakuja baada ya wadau kadhaa wa ngumi kuomba mabondia hao warudiane walipoonyesha baada ya wachezaji hao kuonesha ujuzi na kiwango cha ushindani katika mpambano wao wa Desemba 26 mwaka 2012 kwenye uwanja wa Sheikh Amri Abeidi jijini Arusha wakati wa Boxing Day.
Baada ya mpambano huo, IBF itampatia Francis Cheka nafasi ya kugombea mkanda wa IBF wa Kimataifa (IBF International Super Middleweight) na mabondia wa Ulaya au Marekani. Hii ni kudhihirisha kuwa Francis Cheka hana tena mpinzanai nchini Tanzania na kumpambanisha na mabondia wa kitanzania ni kumpotezea muda na uwezekano wake wa kutengeneza jina na pesa.
Wakati huo huo bondia Thomas Mashali bado ni bingwa wa Afrika ya Mashariki na Kati (ECAPBF) katika uzito wa Middle kwani mkanda wake haukuwa kati ya mikanda iliyogombewa kwenye mpambano uliomalizika Mei mosi.

No comments:

Post a Comment