Wednesday, May 8, 2013

VIFUSI VYATIBUA MANDHARI YA WAKAZI WA IWAMBI


Hii ni sehemu ya vifusi vilivyotelekezwa kwenye barabara za mitaa ya Iwambi jijiniMbeya.
Tatizo hili limeonekana kuwa kero kwa wakazi wa eneo hilo na malalamiko yao kuhusiana na vifusi hivyo yanaonekana kupuuzwa na uongozi wa Halmashauri ya jiji la Mbeya linalotakiwa kuvisambaza ili kuwezesha vyombo vya usafiri vinapita kirahisi.
Hali hii ndivyo ilivyo kwenye barabara za mitaa ya Iwambi
Hali hii kwenye barabara hii hadi sasa ni zaidi ya majuma manne tangu vimwagwe kwenye eneo hili na haijafahamika ni kwa nini.
Jiji fanyeni linalowezekana ili kuwaondolea adha hii wakazi wa Iwambi, mlianza vizuri imekuaje mmekwama kiasi hoiki? Huu sasa ni uchafu ni vyanzo vya magonjwa likiwemo tatizo la kifua kikuu.
Mtandao huu utaendelea kulifuatilia jambo hili kwa wahusika ili kubaini kulikoni.


No comments:

Post a Comment