Na Steve Jonas, Chunya
CHAMA kinachosimamia
zao la Tumbaku Wilayani Chunya (CHUTCU) kinatarajia kupata mkopo wa zaidi ya
Dola 10 Mil. za kimarekani kwa ajili ya
kununua na kusambaza pembejeo katika msimu wa 2013/2014.
Hayo yalisomwa hivi karibuni kwenye Risala ya Chama hicho
wakati wa sherehe za uzinduzi soko la
Tumbaku zilizofanyika Lupatingatinga Wilayani humo katika mkoa wa Mbeya.
Risala hiyo ilisema CHUTCU katika msimu wa 2013/2014 kinategemea
kupata mkopo wa dola 13,402,962.08 kutoka kwenye Benki CRDB wakati NMB itatoa
dola 4,514,785.15 mikopo ambayo itatumika kujengea Mabani ya kisasa na majiko
yake, kusogeza kuni, kuchambulia Tumbaku, ujenzi wa maghala mapya kwenye vyama shiriki vilivyoomba.
Zilitajwa shughuli zingine kuwa ni ununuzi wa pembejeo na
kusambaza kwenye vyama vya msingi vinavyounda CHUTCU ili kuwafikia wakulima kwa
urahisi.
Ilielezwa kwamba zao hilo msimu huu litauzwa kwa wastani wa
Dola 2.6 kwa kilo na bei ya juu itauzwa dola 3.299 kila kilo moja badala ya
dola 1.91bei iliyotumika msimu uliopita.
Taarifa hiyo ilisema
mavuno ya tumbaku msimu wa 2012/2013 hayatafikia malengo kutokana na mabadiliko
ya hali ya hewa yaliyojitokeza kwa mvua kunyesha chini ya kiwango na malengo
yalikuwa ni kupata kilo 12,500,000.
Ilifafanuliwa kuwa katika msimu wa 2013/2014 uzalishaji wa
tumbaku utaongezeka hadi kufikia 13,055,000 kutokana na kuongezeka kwa mahitaji
kufuatia Serikali kuongeza mnunuzi mwingine kutoka Jamhuri ya watu wa China.
Uzalishaji wa tumbaku Wilayani humo msimu wa 2009/2010
ulifikia kilo 377,579, 2010/2011 kilo 628,606, 2011/2012 uzalishaji ulishuka
hadi kilo 354,276 wakati msimu wa
2012/2013 kwa mujibu wa tathimini ya zao (Crop Survey) zitavunwa kilo 578,989.
Kwa mujibu wa Risala hiyo iliyosomwa na Meneja Mkuu
aliyefahamika kwa jina la Bw. Kassia, Chama hicho kimekuwa kikihimiza vyama vya
msingi na wakulima ili misitu isiharibiwe kwa matumizi ya kilimo hicho ambapo
hadi kufikia 2012/2013 jitihada hizo zimefanikiwa kupanda miti2,227,759 kwenye
maeneo mbalimbali Wilayani humo.
Alisema mafanikio hayo yamechangiwa pia na Makampuni mawili ya
Tanzania Leaf Tobaco Company Ltd ambayo ina Vyama vya msingi nane na Premeium Active Tanzania Ltd ambayo
ina vyama 13, Makampuni hayo ni wanunuzi wa zao hilo.
No comments:
Post a Comment