MWALIMU mstaafu wa
elimu ya msingi mkoani Mbeya Bw.Paul Lyambwa Mbamba (74) mkazi wa kijiji cha
Lusungu katika Halmashauri ya Wilaya ya
Mbeya, hivi karibuni alikabidhiwa
kadi ya uanachama wa Chadema baada ya kurudisha kadi ya CCM chama alichokitumikia tangu mwaka 1977
Bw.Mbamba ameuambia mtandao wa www.mamboyakwetu.blogspot.com mjini hapa hivi karibuni kuwa ameamua
kujiunga na CHADEMA baada ya kuchoshwa na CCM kwa vitendo vya unyanyasaji ambavyo amevivumilia kwa kipindi kirefu wakati
akikitumikia Chama hicho.
Katibu wa CHADEMA tawi la Lusungo Bw.Gabriel Songa alithibitisha kuwa ,Bw.Mbamba alirudisha kadi yenye Na.155861 ya CCM ambayo
alikuwa ameilipia ada kwa mara ya mwisho
mwezi Machi 25 mwaka 2010 kwenye tawi la Kasale kijiji cha Idiga kilichopo
kwenye kata ya Bonde la Songwe jimbo la Mbeya Vijijini.
Bw.Songa alisema kuwa,Bw.Mbamba ambaye ana
taaluma ya ualimu baada ya kukabidhi kadi hiyo ya CCM alikabidhiwa kadi ya
CHADEMA yenye Na.CDM 0443364 mnamo Mei 26 mwaka huu na kuthibitisha kwamba
Bw.Mbamba tayari amekuwa mwanachama hai wa Chadema
Katika mahojiano mafupi na Mtandao huu Mbamba alisema kuwa
ndani ya CCM kuna baadhi ya watu wanajifanya miungu watu ambapo wanataka
kunyenyekewa na kukiendesha chama katika misingi ya urafiki na undugu kitendo
ambacho kinasababisha wananchi kuongozwa na watu ambao si chaguo lao.
Mwalimu huyo alisema kwamba ,kwenye uanachama wake ndani ya
CCM aliwahi kugombea nafasi ya udiwani katika kata hiyo kwenye uchaguzi mkuu
uliopita ambapo alisema kuwa alifanyiwa kitu mbaya vikiwemo vitendo vya
kutishia uhai wake ambavyo vilikuwa vikifanywa na wanachama wa CCM hata kusababisha kutupwa katika uchaguzi huo.
Aliongeza kuwa ndani ya CCM hakuna Demokrasia ya kweli bali
imejaa unafiki na vitendo vya ubabe ambavyo havina tija katika shughuli za
maendeleo ya watanzania.
No comments:
Post a Comment