MWENYEKITI WA WAFUGAJI BONDE LA SONGWE AKIZUNGUMZIA KADHIA WANAYOIPATA KUTOKA KWA WATENDAJI WA SERIKALI YA WILAYA YA CHUNYA
RISTI AMBAZO ZINATOLEWA
KAMA KAWA, NDUGU..........WANATOZWA MILIONI 6, STAKABADHI ZINAANDIKWA LAKI 6
WAFUGAJI WAKIUZA MIFUGI YAO MNADANI ..................BONDE LA SONGWE.......
STAKABADHI BADALA YA KUANDIKWA MIFUGO KUZIDI ZINAANDIKWA KULISHA MASHAMBA AMBAYO HAYAJULIKANI NI MASHAMBA YA NANI NA ENEO GANI!
RISTI AMBAZO ZINATOLEWA
KAMA KAWA, NDUGU..........WANATOZWA MILIONI 6, STAKABADHI ZINAANDIKWA LAKI 6
WAFUGAJI WAKIUZA MIFUGI YAO MNADANI ..................BONDE LA SONGWE.......
·
BAADHI
ya watendaji wa Serikali wilayani Chunya wameamua kupimana nguvu na
Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya ufundi Philip Mulugo ambaye ni
Mbunge wa Jimbo la Songwe kwa kuwakamata wafugaji wa Jimbo hilo na
kuwatoza faini zisizo na tija.
Hali hiyo imebainika baada ya kikosi cha waandishi wa habari kutembelea jimbo hilo
na kukutana na vilio vya wananchi hasa wafugaji ambao walisema kuwa
watendaji hao wanaongozwa na Afisa Mifugo wa wilaya hiyo Adam Mbale.
Mwenyekiti
wa wafugaji wahamiaji wa bonde la Songwe Julius Machia alisema tangu
zoezi la kukamata mifugo inayozidi 70 na kutozwa kwa kila mfugo
unaozidi shilingi 20,000 kumesababisha matatizo mengi kwa wafugaji
yakiwemo baadhi yao kuuwawa na askari kwa kupigwa risasi katika
operesheni ya kamata mifugo na wafugaji kudhulumiwa kwa kupigwa faini
kubwa hali ambayo inamlazimu mfugaji kuuza mifugo kwa bei ya hasara.
“Kwa
miaka 10 sasa zoezi la kukamata mifugo, limekuwa kama mvuta sigara
huvuta sigara anapojisikia kiu kwa kuwa watendaji wa serikali
wanaendesha zoezi hili bila mpangilio na limekuwa linafanyika mara kwa
mara tena kwa unyanyasaji mkubwa’’,anasisitiza Machia.
Wafugaji
hao walisema mbali na fedha wanazotozwa pia kuna vitendio vya
udhalilishaji na ambavyo havifuati haki za binadamu vikiwemo kutishiwa
risasi hewani ili wenye mifugo wajifiche na kuogopa kuuwawa,kupiga
nyumba risasi hadi kubomoa ambapo walitolewa mfano nyumba ya mfugaji
Jikolela Mihambo wa kijiji cha Swela nyumba yake iliteketea kwa moto
baada ya kupigwa kwa risasi.
Mfugaji
katika kijiji cha Chang’ombe Gamaya Bunga alisema utozwaji wa faini
unaonekana kufanyika kwa upendeleo kwa kuwa wakulima wanaovunja sheria
na kulima kwenye maeneo ambayo hayaruhusiwi kisheria kama vile kwenye
vyanzo vya maji vya mto Songwe na ziwa Rukwa hawakamatwi.
Baadhi ya risiti ambazo MTANDAO WA kalulunga.blogspot.com imezipata
nakala zake zinaonesha kuwa mfugaji Materemki Lugola wa kijiji cha
Wanzani alilipa faini ya shilingi milioni 4,740,000 mwaka 2001 kwa
ajili ya mifugo 948 kula katika mashamba ya wakulima badala ya faini
ambazo zimetakiwa za kuwa na mifugo mingi.
Aliyetakiwa kupokea fedha hizo ni mkulima ambaye shamba lake limeliwa
na mifugo kupitia ofisi za vijiji badala yake mpokeaji wa fedha hizo ni
Afisa mifugo,kilimo na ushirika wa Halmashauri ya wilaya ya Chunya
ambaye amesaini katika risiti kuwa amepokea kiasi hicho cha fedha.
Risiti
nyingine ya mwezi Mei mwaka 2011 inaonesha kuwa mfugaji Julius Machia
wa kijiji cha Chang’ombe alilipa faini ya shilingi milioni sita kwa
ajili ya kuzidi mifugo 300 ambapo kila mfugo uliozidi ulitozwa shilingi
20,000,hata hivyo risiti hiyo imeandikwa mfugaji huyo amelipa shilingi
laki sita badala ya milioni sita.
Wafugaji
wahamiaji wengine waliopigwa faini ya kuzidi kwa mifugo na kuandikiwa
risiti kuwa ni faini kwa ajili ya kulisha mifugo kwenye mashamba ni
Misa Njigula wa kijiji cha Totowe ambaye alipigwa faini ya shilingi
1,275,000 kwa ajili ya ng’ombe 255,Masale Gidai wa kijiji cha Magamba
alipigwa faini ya shilingi 770,000.
Masele
Julius wa kijiji cha Ifuko alipigwa faini ya shilingi 140,000,Mashala
Kwilasa wa kijiji cha Galula Sh. 115,000 na mfugaji John Kasema wa
Totowe Sh. milioni nane kwa ng’ombe 400.
Kwa
upande wake afisa mifugo,kilimo na ushirika katika Halmashauri ya
wilaya ya Chunya Adamu Mbale alisema kuwa Kutokana na uwepo wa mifugo
mingi serikali mwaka 2002 ilitoa sheria ya Halmashauri ya wilaya ya
Chunya kuhakikisha kila mfugaji katika bonde hilo awe na mifugo
isiyozidi 70 na kwamba mfugaji atakayezidisha kiwango hicho cha mifugo
anapigwa faini ya shilingi 20,000 kwa kila mfugo unaozidi.
“Kuna
watendaji wawili kutoka vijiji vya Bonde la Songwe ambao wamechunguzwa
na TAKUKURU baada ya kubainika kufanya udanganyifu kwenye risiti za
malipo na kesi zao zipo mahakamani’’,anasema Mbale.
Beston
Mwambene mwalimu mkuu wa shule ya msingi Ihovyo anasema“Wafugaji
wanaamini kuwa kutajirika kwao ni kuongeza mifugo na sio kupunguza
mifugo kwa kuwa hata wakulima wanakuwa na maisha bora kwa kuongeza
uzalishaji katika mashamba yao hapa kinachotakiwa waelimishwe zaidi kuwa na mifugo bora’’,anasema Mwambene.
Kwa upande wake Mbunge wa Jimbo hilo
Philip Mulugo ambaye ni Naibu waziri wa elimu na mafunzo ya ufundi
alipoulizwa kwa njia ya simu alisema kuwa alikuwa jhana taarifa hivyo
aliahidi kulifuatilia jambo hilo ambapo watumishi hao wamefanya tena zoezi hilo Mei 16 mpaka Juni 1, mwaka huu huku wakitoza mpaka mbuzi Sh. 20,000.
No comments:
Post a Comment