Tuesday, July 30, 2013

BABA AMVUA CHUPI MWANAE NA KUNGIJINGIJI NAYE MIAKA MINNE KISHA MIMBA



 


Pichani ni Yusufu Amani (39) mkazi wa Isanga jijini Mbeya aliyezaa na mwanaye wa kumzaa baada ya kuzini na bintiye miaka mine mfululizo.
Yusufu hapa akijifunika asipigwe picha baada ya hukumu yake
Mtoto aliyebakwa na baba yake (mwenye mtoto mgongoni) akiwa na  mama yake mzazi ambaye aliktengana kwenye ndoa na mtuhumiwa.Hapa walikuwa wakitoka kwenye jingo la mahakama Kuu jijini Mbeya.

Mwendesha mashtaka wa Serikali katika mahakama ya Wilaya, Achiles Mulisa aliiambia Mahakama hiyo mbele ya Hakimu Gilbert Ndeuruo kuwa mshitakiwa huyo alianza kumwingilia kimwili binti yake (jina linahifadhiwa) akiwa na umri wa miaka 12 na na kitendo hicho kiliendelea kwa miaka minne mfululizo kisha kumpachika mimba.

Hakimu alisema kitendo hicho kilifanyika baada ya Yusufu kutengana na mke wake mwaka 2008 wakati huo binti huyo akiwa darasa la 5 kwenye shule moja mkoani humo hadi binti alipobainika kuwa na mimba mwezi Mei 2012.

Alisema kitendo hicho ni kinyume cha sheria kifungu 154 (1) 155 sura ya 16 iliyofanyiwa marekebisho mwaka 2002 pamoja na kifungu 158 (a) cha makosa ya kuzini.

Alisema mtuhumiwa mbinu alizotumia ili mtot asivujishe siri  ilikuwa ni vitisho na alipo gungua kwamba binti ana mimba alimshawishe asimtaje badala yake amtaje kijana yeyote wa mtaani hapo.

Hakimu Ndeuruo alisema kuwa Mahakama inamtia hatiani mtuhumiwa kutokana na ushahidi uliotolewa na mhanga pamoja na ushahidi wa kitaalamu kutoka kwa Mkemia Mkuu wa Serikali.

Alisema ushahidi huo ni wa Vina saba kutoka kwa mtuhumiwa, mhanga na mtoto aliyezaliwa (mjukuu wa Yusufu wa kutoka maungoni mwa binti yake) , ushahidi huo uliotoka kwenye maeneo 15 ulieleza kuwa mshitakiwa ni baba halali wa kichanga huyo baada ya vipimo kufungana kwa asilimia 99.9.

Lakini katika hali ya kushangaza Yusufu alipopatiwa nafasi ya kujitetea ili apunguziwe adhabu au asiweze kuhukumia alisema hana cha kujitetea na vyovyote itakavyokuwa kwake ni shwari isipokuwa alihitaji apatiwe nakala ya hukumu yake.

 

Baadae Hakimu alimhukumu kwenda kutumikia jela kifungo cha miaka 30 na kusema mshitakiwa ana haki ya kukata Rufaa katika Mahakama Kuu kama hakuridhika na hukumu hiyo.


Awali ushahidi wa mshitakiwa Mahakamani hapo ulieleza kuwa Yusufu hakutenda kosa hilo bali alitengenezewa kesi na mkewe ambaye tayari anaishi na mume mwingine jambo ambalo Hakimu alilitupilia mbali na kusema mfa maji haishi kutapatapa.


 
 



Saturday, July 13, 2013

WAFANYABIASHARA WAILAUMU JIJI LA MBEYA



Na Anna Livifile, Mbeya

WAFANYABIASHARA wa Soko la Sido jijini hapa wamelitupia lawama uongozi wa jiji la Mbeya wakidai hawanufaiki na mapato ya soko kwa kufuatia mapungufu yaliyopo sokoni hapo.

Kwa mujibu wa katibu wa soko hilo Bw. Alanus Ngogo wafanyabiashara wanatozwa ushuru kila siku sh. 300 kwa kila mmoja kati ya wafanyabiashara 1114 lakini mbali ya Halmashauri ya jiji kukusanya kiasisi kikubwa cha fedha soko hilo limekuwa likikabiliwa na miundo mbinu finyu.

Bw. Ngogo aliyataja baadhi ya mapungufu yaliyopo sokoni hapo kuwa ni kukosekana kwa umeme, taka kutozolewa kwa wakati, barabara za kuingia na kutoka kwa magari yanayopeleka mahitaji ya wafanyabiashara na mifereji ya kupitishia maji machafu.

Alisema tatizo lingine ambalo limekuwa kero kwa watumiaji wa soko hilo ni kukosekana kwa vyoo ambapo wanalazimika kutumia vyoo vya kulipia vinavyo milikiwa na watu binafsi kitendo ambacho kimeibua manung’uniko na kuhoji ni vipi jiji limeshindwa kuweka huduma hizo ikilinganishwa na ukusanyaji wa mapato.

Vilevile alishauri kuwa kuwepo na sehemu maalumu kwa ajili ya matangazo yatakayoonesha kupanda na kushuka kwa bei za bidhaa zinazopatikana sokoni hapo kinyume na sasa ambapo hakuna utaratibu huo na kuwepo mkanganyiko kati ya wafanyabiashara na wanunuzi.

Katibu huyo alilitaka jiji lilitambulishe soko kwenye taasisi mbalimbali nchini ili wafanyabiashara waweze kupata mikopo itakayo kuza mitaji na kipato chao pia kuliwezesha jiji kuongeza vyanzo vya mapato

Katika hatua nyingine kiongozi huyo alisema kuwa wafanyabiashara wanataka kusikia kauli ya jiji itakayowatambulisha kuahamia soko jipya lililopo Mwanjelwa jijini hapa kwa maelezo kuwa wamesubiri kwa muda mrefu.

Soko hilo lipo katika hatua za mwisho za ujenzi tangu lilipoungua zaidi ya miaka mnne iliyopita hali iliyo sababisha wafanyabiashara hao kuhamia kwenye soko la Sido kwa muda ili kupiha shughuli za ujenzi wa soko jipya.

Mwisho………….


Wednesday, July 3, 2013

CHUTCU KINATARAJIA KUPATA MKOPO WA ZAIDI YA MIL.1O

Na Steve Jonas, Chunya

CHAMA   kinachosimamia zao la Tumbaku Wilayani Chunya (CHUTCU) kinatarajia kupata mkopo wa zaidi ya Dola 10 Mil. za kimarekani  kwa ajili ya kununua na kusambaza pembejeo katika msimu wa 2013/2014.

Hayo yalisomwa hivi karibuni kwenye Risala ya Chama hicho wakati wa sherehe za uzinduzi  soko la Tumbaku zilizofanyika Lupatingatinga  Wilayani humo katika mkoa wa Mbeya.

Risala hiyo ilisema CHUTCU katika msimu wa 2013/2014 kinategemea kupata mkopo wa dola 13,402,962.08 kutoka kwenye Benki CRDB wakati NMB itatoa dola 4,514,785.15 mikopo ambayo itatumika kujengea Mabani ya kisasa na majiko yake, kusogeza kuni, kuchambulia Tumbaku, ujenzi wa maghala mapya kwenye vyama  shiriki vilivyoomba.

Zilitajwa shughuli zingine kuwa ni ununuzi wa pembejeo na kusambaza kwenye vyama vya msingi vinavyounda CHUTCU ili kuwafikia wakulima kwa urahisi.

Ilielezwa kwamba zao hilo msimu huu litauzwa kwa wastani wa Dola 2.6 kwa kilo na bei ya juu itauzwa dola 3.299 kila kilo moja badala ya dola 1.91bei iliyotumika msimu uliopita.

 Taarifa hiyo ilisema mavuno ya tumbaku msimu wa 2012/2013 hayatafikia malengo kutokana na mabadiliko ya hali ya hewa yaliyojitokeza kwa mvua kunyesha chini ya kiwango na malengo yalikuwa  ni kupata kilo 12,500,000.

Ilifafanuliwa kuwa katika msimu wa 2013/2014 uzalishaji wa tumbaku utaongezeka hadi kufikia 13,055,000 kutokana na kuongezeka kwa mahitaji kufuatia Serikali kuongeza mnunuzi mwingine kutoka Jamhuri ya watu wa China.

Uzalishaji wa tumbaku Wilayani humo msimu wa 2009/2010 ulifikia kilo 377,579, 2010/2011 kilo 628,606, 2011/2012 uzalishaji ulishuka hadi kilo 354,276 wakati  msimu wa 2012/2013 kwa mujibu wa tathimini ya zao (Crop Survey) zitavunwa kilo 578,989.

Kwa mujibu wa Risala hiyo iliyosomwa na Meneja Mkuu aliyefahamika kwa jina la Bw. Kassia, Chama hicho kimekuwa kikihimiza vyama vya msingi na wakulima ili misitu isiharibiwe kwa matumizi ya kilimo hicho ambapo hadi kufikia 2012/2013 jitihada hizo zimefanikiwa kupanda miti2,227,759 kwenye maeneo mbalimbali Wilayani humo.

Alisema mafanikio hayo yamechangiwa pia na Makampuni mawili ya Tanzania Leaf Tobaco Company Ltd ambayo ina Vyama vya msingi  nane na Premeium Active Tanzania Ltd ambayo ina vyama 13, Makampuni hayo ni wanunuzi wa zao hilo.

Wednesday, May 8, 2013

JESHI LA POLISI MKOANI MBEYA LIMEPONGEZWA

Na Steve Jonas 
JICHO LANGU BLOGU
 WANANCHI Mkoani Mbeya wamelipongeza Jeshi la Polisi katika jitihada zinazofanywa ili kudhibiti matukio ya uhalifu likiwemo tukio la hivi karibuni la kuwateketeza majambazi watano katika majibizano ya silaha za moto mchana kweupeeee mkoania hapa.
Polisi katika majibizano hayo walifanikiwa kuwaua watu watano waliosadikika kuwa ni majambazi, tukio hilo lilitokea kwenye kijiji cha Garijembe nje kidogo ya jiji la Mbeya hizo zimekuja Siku moja baada ya Jeshi hilo kuwauwa watu watano
  
Katika kuhakikisha Jeshi hilo linaendelea  kufanya kazi katika mazingira mazuri na kwa mafanikio  na kuunga mkono juhudi zao, Wadau mbali mbali  leo  wamejitokeza kulichangia jeshi hilo katika Hafla iliyofanyika katika viwanja vya ofisi ya Kamanda wa Polisi Mkoani hapa.
  
Hafla hiyo ambayo mgeni rasmi alikuwa ni Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wa Mbeya  pia ni Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Abbas Kandoro Jumla ya Shilingi Milioni 28 zilipatikana vikiwemo vifaa mbali mbali.
  
Mwenyekiti wa kikosi cha Mafanikio cha kuchangisha fedha na michango ya kuliwezesha Jeshi la Polisi kufanya kazi katika Mazingira mazuri, Julius Kaijage amesema Askari wa Jeshi la Polisi wanafanya kazi katika mazingira magumu hivyo ni jukumu la kila mwananchi kuhakikisha analiwezesha kwa hali na mali.
  
Katika Hafla hiyo Jumla ya Pikipiki tano zilinunuliwa kati ya pikipiki hizo tatu zimetolewa na Benki ya NMB kwa thamani ya Shilingi za kitanzania Milion 5.4, wakati kamati ya ulinzi ilinunua pikipiki Mbili kwa Thamani ya Shilingi Milioni Moja na Laki Nane.
  
Mbali na michango hiyo pia Wakala wa Majengo mkoa wa Mbeya (TBA) imetoa mabati 22 ya Geji 28 yenye thamani ya Shilingi 460,000/=, pia kamati ya Mafanikio imenunua Matairi nane yenye thamani ya Shilingi Milioni 3,020,000/=,pamoja na mafuta kwa ajili ya magari ambayo ni Lita 360 kwa Mwaka zilizoahidiwa na kampuni ya G4S.
  
Mbali na pongezi hizo Wananchi hao wamemshauri Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya Diwani Athumani mbali na kupambana na uhalifu katika Mkoa wa Mbeya na kuwasisitiza watu wanaofanya shughuli zisizokuwa na uhalali kuacha mara moja au kuhama Mkoa pia wapendekeza kufanya ziara za kushtukiza katika Vituo vidogo vya Polisi.
Kwa upande wake Kamanada wa Polisi Mkoani hapa Diwani Athumani amewapongeza wadau mbalimbali waliojitokeza kulisaidia jeshi hilo ambapo amewahahakikishia wananchi wa mkoa huu kuwa kwa sasa mkoa wa mbeya upo katika mazingira salama kutokana na ushirikiano uliopo kati ya wananchi na jeshi hilo .


Meneja wa Benki ya NMB kanda ya nyanda za juu kusini Bi.Lucresia Makirie akimkabidhi pikipiki tatu
Mwenyekiti wa kikosi cha Mafanikio cha kuchangisha fedha na michango ya kuliwezesha Jeshi la Polisi kufanya kazi katika Mazingira mazuri, Julius Kaijage
Mwenyekiti wa kikosi cha Mafanikio Julius Kaijage akimkabidhi pikipiki mbili na matairi 4 ya gari pamoja na mabati mkuu wa mkoa wa Mbeya Abas Kandoro vifaa hivyo vyote vimetoka kwa wadau wa ulinzi mkoani hapa
Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wa Mbeya ambaye pia ni Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Abbas Kandoro akiongea na wadau mbali mbali kwenye hafla fupi ya kupokea misaada toka kwa wadau wa ulinzi mkoani hapa
Mwenyekiti wa kikosi cha Mafanikio cha kuchangisha fedha na michango ya kuliwezesha Jeshi la Polisi kufanya kazi katika Mazingira mazuri, Julius Kaijage amesema Askari wa Jeshi la Polisi wanafanya kazi katika mazingira magumu hivyo ni jukumu la kila mwananchi kuhakikisha analiwezesha kwa hali na mali.
Meneja wa Benki ya NMB kanda ya nyanda za juu kusini Bi.Lucresia Makirie amesema benki yake imetoa msaada Pikipiki tatu kusaidia jeshi hilo ili zisaidie katika ulinzi shirikishi katika mkoa wa Mbeya
Kamanada wa Polisi Mkoani Mbeya Diwani Athumani amewapongeza wadau mbalimbali waliojitokeza kulisaidia jeshi hilo ambapo amewahahakikishia wananchi wa mkoa huu kuwa kwa sasa mkoa wa mbeya upo katika mazingira salama kutokana na ushirikiano uliopo kati ya wananchi na jeshi hilo .

VIFUSI VYATIBUA MANDHARI YA WAKAZI WA IWAMBI


Hii ni sehemu ya vifusi vilivyotelekezwa kwenye barabara za mitaa ya Iwambi jijiniMbeya.
Tatizo hili limeonekana kuwa kero kwa wakazi wa eneo hilo na malalamiko yao kuhusiana na vifusi hivyo yanaonekana kupuuzwa na uongozi wa Halmashauri ya jiji la Mbeya linalotakiwa kuvisambaza ili kuwezesha vyombo vya usafiri vinapita kirahisi.
Hali hii ndivyo ilivyo kwenye barabara za mitaa ya Iwambi
Hali hii kwenye barabara hii hadi sasa ni zaidi ya majuma manne tangu vimwagwe kwenye eneo hili na haijafahamika ni kwa nini.
Jiji fanyeni linalowezekana ili kuwaondolea adha hii wakazi wa Iwambi, mlianza vizuri imekuaje mmekwama kiasi hoiki? Huu sasa ni uchafu ni vyanzo vya magonjwa likiwemo tatizo la kifua kikuu.
Mtandao huu utaendelea kulifuatilia jambo hili kwa wahusika ili kubaini kulikoni.


FRANCIS CHEKA APONGEZWA NA IBF




http://www.gushit.com/files/bookmark_photos/abcffd70f4L.jpgShirikisho la Ngumi la Kimataifa (IBF) limempongeza bondia wa kitanzania, Francis Cheka kutokana na uwezo mkubwa alionao kwenye ndondi katika uzito Super Middle wa viwango vya kimataifa.
 Cheka alifanikiwa kutetea mkanda wake wa IBF Africa katika uzito huo baada ya kumshinda kwa KO bondia Thomas Mashali a.k.a “Simba asiyefugika” Mei Mosi mwaka 2013 katika ukumbi wa PTA jijini Dar Es Salaam.
IBF imefikia hatua ya kumpongeza mwanamasumbwi huyo baada ya ushindi huo ambao umedhihirisha kuwa yeye  ni bingwa wa bara la Afrika na anatazamiwa kurudiana na bondia wa Malawi Chimwemwe Chiotcha mnamo Agosti katika mpambano la kutetea mkanda wake.
Mpambano huo wa marudiano utafanyika katika jiji la Blantyre nchini Malawi na tayari majadiliano ya  yanaendelea vizuri na Kampuni ya “Mawenzi Boxing Promotion” ya nchini Malawi ikisimamiwa na Stephen Mawezni ndiyoitakayoandaa mpambano huo. 
Pambano hili linakuja baada ya wadau kadhaa wa ngumi kuomba mabondia hao warudiane walipoonyesha baada ya wachezaji hao kuonesha ujuzi na kiwango cha ushindani katika mpambano wao wa Desemba 26 mwaka 2012 kwenye uwanja wa Sheikh Amri Abeidi jijini Arusha wakati wa Boxing Day.
Baada ya mpambano huo, IBF itampatia Francis Cheka nafasi ya kugombea mkanda wa IBF wa Kimataifa (IBF International Super Middleweight) na mabondia wa Ulaya au Marekani. Hii ni kudhihirisha kuwa Francis Cheka hana tena mpinzanai nchini Tanzania na kumpambanisha na mabondia wa kitanzania ni kumpotezea muda na uwezekano wake wa kutengeneza jina na pesa.
Wakati huo huo bondia Thomas Mashali bado ni bingwa wa Afrika ya Mashariki na Kati (ECAPBF) katika uzito wa Middle kwani mkanda wake haukuwa kati ya mikanda iliyogombewa kwenye mpambano uliomalizika Mei mosi.

Tuesday, February 5, 2013

RADI YAUA WATU WATANO MBEYA





WATU watano wamefariki dunia mkoani Mbeya kwa kupigwa radi katika matukio matatu tofauti likiwemo lililoua ndugu watatu wa familia moja. 
 
Wanandugu hao watatu wakazi wa kata ya Nyimbili Wilayani Mbozi wamefikwa na mauti leo majira ya saa saba mchana wakati mvua kubwa iliyoambatana na radi za mara kwa mara ikiendelea kunyesha wakiwa nyumbani. 

Afisa mtendaji wa kata ya Nyimbili Lingtone Nzowa amewataja waliopoteza maisha kuwa ni Jerumana Halinga (35), David Halinga (5) na Kumi Halinga(3) na mtoto wa miezi tisa ambaye hakufahamika mara moja jina lake, alijeruhiwa katika ajali hiyo. 
 
 Tukio la pili limetokea katika kijiji cha Magurula kata ya Utengule Usangu Wilayani Mbarali ambapo radi iliyotokana na mvua kubwa imempiga Kasim Sagutangu na kusababisha kifo chake, Diwani wa kata hiyo Juntwa Mwalyaje amesema mvua hiyo imenyesha Februari 3 majira ya saa nane za mchana.
Tukio la tatu lilitokea Februari 3 katika kijiji cha Mbagala Kata ya Ilembo kwenye Halmashauri ya Wilaya ya Mbeya mwanamke Kotanida Petro alifariki dunia baada ya kupigwa na radi akiwa shambani kwake.
 
 Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Mbeya, Diwani Athumani amethibitisha kutokea kwa matukio hayo ya vifo vya watu watano vilivyotokana na radi.