Wednesday, April 25, 2012

BEZ M'AMY AIMS TO SUPPORT ORPHANS IN AFRICA

 
BEZ M'AMY which in English means ' ' without mother '' is a charitable, non-for- profit, on governmental organization founded in the Czech republic in 2006 by Ondrej Horecky and his wife Tereza Horecka.

This organization was registered at the ministry of interior, with registration number.27036847.


The new board, which was created in 2010, consists of five members, each of them having his/her own experience with work in Tanzania.


The chairman of the organization is Toma's Gongol, while two other members of the board are Michal Sot'ak and Michaela Gongolova.


Horecky continues being an active, member being involved in most of the projects, and Chris Zacharia who joined Bez M'amy in 2011 continues to be the organizations representative in Africa.


The main objective of the organization is to help and support children in Africa, especially orphans.


Due to the HIV/AIDS the number of children living without their parents is increasing every year.


Zacharia who is an African representative told the Guardian in an interview conducted recently in Mbeya that, these children are usually taken care of by their closest relatives, grandparents, uncles, aunties etc.


He said the children themselves some times suffer from lack of food and money as well, and thus the poverty of all deepens.


''We believe that with our love and dedication the children will be better prepared for their future lives'', Zacharia remarked.


He said apart from providing regular meals, healthcare and education, their main goal is to support the children so that they can grow to independent and adults wi8th are healthy and proper approach to life.


Zacharia further pointed out that hand in hand with this key idea there are other supporting targets, which should create an environment favorable for achieving the main objective.


'' We therefore strive to support local communities so that they become self dependent, especially in the healthcare and processing of the natural resources, but also help the people without their own sources of income or necessary Medicaments, and support the local Christian communities'' he said.

                           OPERATING AREA

We are focusing on the Mbeya region which is in Tanzania, East Africa.


Mbeya is the provincial capital which lies at 1700 meters above sea level.


The main tribes are the Nyakyusa, Safwa, Nyiha, Ndali, Malila, Bungu and Wasangu.


Approximately 60 kilometers east of the town there is a farmers village known as Mahango, where there is no electricity, good roads or regular access to water, and this is the place where we are based and work.

                                OUR ACHIEVEMENT

We have managed to achieve a good deal of work in Mahango since the creation of the organization.


First of all a missionary house has been built, which serves as a center for the local congregation of the catholic nuns ''sisters of our lady queen of the Apostles.

The main goal of the nuns is to take care of the orphans, their education and healthcare, and without their life –long sacrifices and love we would not be able to operate in Africa at all.

Next to the missionary house we have built a small orphanage hosting 8 children, and at the moment we are raising funds to extend the orphanage.

‘’We are currently building two larger dormitories, one for  the boys and another one for girls, each providing living for up to 70 children’’ said Zacharia.

The money spent on these projects alone amounts to about Mil.90 /=,and the next project which will consist on building a Dinning room, Kitchen and a store will spend about Mil.29/=.

To make sure we achieve our goal in a short time and help as many children as possible we decided to register another local organization in Tanzania without mother organization (WMO) with 12 local members from Mbeya especially in Mahango and our African representative Zacharia became the chairman of WMO.

Bez m’amy supports about 53 orphans in Mbeya region at Mahango Village, and few are in Sumbawanga, Rukwa region.

WMO was registered in Tanzania by the Ministry of home Affairs, with registration number S.A18016 in February 2012.
WMO closely supervisor daily activities of our projects in Tanzania, and with their cooperation between Bez m’amy and WMO we have seen the fast moving and success of the planned projects.

            SCHOOL PROJECTS AT KAJUNJUMELE

It is not enough to provide food, clothing and a shelter for the orphans, but it is crucial to arrange suitable education, healthcare and prepare them so that they can integrate into the society.

In the cooperation with the US Embassy we have therefore contributed towards setting up Kajunjumele Nursery School where orphans can come for free and in the age 3-6, who can learn how to read, write and do basic maths.

There is a primary school we support in the nearby village which the children can attend too.

In the framework of the project ‘’school to school’’ we have managed to purchase desks for the schools in Mahango as well as neighboring Simike.

The renovation of some classrooms of Kisa, Galula and Ilasilo primary schools as coasted about Mil.1/= each, and in order to provide further education, more finance is needed, and since 2007 we have been supporting some children at their high school studies.

The money figure which has been mentioned above is being provided every year, while the next project of constructing dormitory number 2 will cost about Mil.55/=.

The complex of our projects should lead to the independent of children, and unlike most other similar organizations we do not have worry about bureaucratic and other expenses.

The total cost of all the projects is more than Mil.150/=

                         

Monday, April 23, 2012



TUKIO la mwalimu wa shule ya msingi ya Juhudi ya jijini hapa  kufukuzwa shuleni hapo akituhumiwa kujihusisha na vitendo vya ushikina mapema mwezi Aprili mwaka huu ,limechukua sura mpya baada ya kubainika baadhi ya wanafunzi pia kujihusisha na vitendo hivyo.

Hayo yalisemwa katika mkutano wa hadhara uliofanyika mnamo Aprili 19 mwaka huu mkutano ambao ulikusudia kuzungumzia mapato na matumizi ya shule hiyo baada ya kutokea mtafaruku kati ya wazazi na kamati ya shule.

Katika mkutano huo, mwenyekiti wa mtaa wa Mwambenja Bw.Lucas Mwakalonge alisema kuwa wanafunzi watatu walikamatwa na walinzi shuleni hapo wakiwa katika harakati za vitendo vya kishirikina.

Bw.Mwakalonge alisema kwamba baada ya wananchi kukusanyika na kujionea tukio hilo waliamuru watoto hao wafikishwe mikononi mwa Polisi ili wakatoe maelezo ambako waliachiwa kwa dhamana baada ya kutoa  maelezo.

Baada ya kugundua kwamba wanafunzi hao  walikuwa wakijihusisha na vitendo vya kishirikina baadhi ya wazazi waliamua kumuomba msamaha mwalimu aliyetajwa kwa jina moja la Kyando ambaye awali alituhumiwa kuhusika na vitendo hivyo kasha kumfukuza shuleni hapo.

Hata hivyo,baadhi ya wananchi bado walionesha dalili za kutokubaliana na suala la kumuomba radhi mwalimu huyo kwa kukosa imani naye.

Mwenyekiti huyo alisema matukio kama hayo si mageni katika mtaa huo kitendo ambacho kimekuwa kikieneza sifa mbaya ya mtaa wa Mwambenja,tukio hilo na lile lililo sababisha mwalimu Kyando kuondolewa shuleni hapo ni sawa na tukio lililo wahi kutokea miaka 15 iliyopita.

Mapema mwezi huu kando kando ya mto jirani na shule vilikutwa vitu vya ajabu ambavyo vilisadikika kuwa ni vitu vya kishirikina,vitu hivyo ni Vibuyu,vyungu viwili,fuvu la kichwa cha ng’ombe,pembe moja la ng’ombe na vitambaa viwili vyenye rangi nyeusi na nyekundu ambavyo vilifungwa kwenye miti miwili tofauti.

Mmoja wa wajumbe waliohudhuria mkutano huo aliyefahamika kwa jina la Frank Jacob,bila ya kufafanua  aliwataka walimu wote wa shule ya Juhudi pamoja na kamati ya shule wakae na kumaliza tofauti zao ambazo zimekuwa zikitapakaza sifa mbaya ndani ya jamii inayo wazunguka.


MBEYA CITY YAWASONONSHA MASHABIKI WA SOKA MBEYA


TIMU ya  Mbeya City ya mkoani hapa  imewasonesha mashabiki  wa soka jijini hapa  baada ya kupokea kichapo cha mabao 2-0 kutoka kwa  timu ya Polisi Morogoro kwenye  mchezo uliochezwa mjini Morogoro,na  kufuta ndoto za kucheza Ligi kuu msimu ujao.

 Mashabiki walioongea  na majira mjini hapa  kwa nyakati tofauti  wamesema  kuwa  kushindwa kupanda daraja kwa timu hiyo ,kumechangiwa na kocha mkuu wa timu hiyo Juma Mwambusi  baada ya kuachiwa madaraka yote ya timu na kujiamini kupita kiasi.

Shabiki  wa soka jijini hapa  Lugano Hezron   alisema kuwa timu hiyo ya Halmashauri ya jiji la Mbeya ,ilkuwa na uwezo wa kupanda daraja kutokana na kusheheni wachezaji wenye vipaji lakini uongozi ndio ulioboronga .

Aliwataja wachezaji hao kuwa ni Venance Muligo,Josephat Maston ambao wana uwezo mkubwa  kiuchezaji lakini waliachwa dakika za mwisho kutokana na sababu zisizojulikana,ambapo nahodha wa timu hiyo Patrick Mangungulu alifukuzwa kambini mjini Morogoro kutokana na utovu wa nidhamu.

Wachezaji wengine ni  Fidel Castro,mlinda mlango Aswile Asukile, Moses Mwazembe,David Mpangala pamoja na wachezaji  ambao ni nguzo kubwa ya timu hiyo,lakini hawakutumiwa vizuri na hivyo kuwakosesha  mashabiki wa Mbeya uhondo wa kuiona ligi kuu kama walivyotegemea kuwa  na timu mbili  za mkoa wa Mbeya City na Prisons zote za jijini hapa.

Mdau mwingine wa soka aliyejitambulisha kwa jina la Shomari Rajabu  alisema kuwa sababu kubwa iliyofanya City wasipande daraja,ni kwamba mwalimu wa timu hiyo  Mwambusi hakuwa na benchi la ufundi lenye uwezo wa kumshauri pale timu hiyo inapo shinda au kufungwa.

Aliongeza kwamba timu hiyo ilkuwa na uwezo mkubwa wa kifedha kiasi kwamba wangeongeza nguvu kwenye benchi  la  ufundi ,ila wakaridhika na uwezo wa kocha mkuu pekee kwa vile timu ilikuwa inashinda .

Mdau huyo  ametoa ushauri kwa timu hiyo kwamba mwakani wakifanikiwa kuingia kwenye hatua  za fainali za ligi daraja la kwanza ,waongeze nguvu katika benchi la ufundi ili washirikiane mwalimu wa timu hiyo.

Shabiki  Geofrey Kilumbi alisema kuwa kushindwa kupanda daraja kwa Mbeya City na kuikosa Ligi kuu msimu ujao,kulitokana na kujiamini kupita kiasi kwa timu hiyo.

Akifafanua zaidi  alisema kuwa hatua hiyo ilitokana na timu hiyo kushinda karibu mechi zote za hatua ya awali ilizocheza za nyumbani na ugenini.
Mwambusi akizungumza kwa njia ya simu kutoka mkoani Morogoro ambako mashinda hayo ya tisa bora yalifanyika , alisema kushindwa kwa Mbeya City kufuzu, kumetokana na wao kukosa uzoefu wa mashindano ya kituo na sio Ligi.
MWISHO

Thursday, April 19, 2012

WALIOVULIWA MADARAKA UVCCM MBEYA KUJIBU KINAGAUBAGA IJUMAA


 





VIONGOZI waandamizi wa UVCCM waliovuliwa uongozi na Baraza kuu la Jumuiya ya Vijana wa CCM (UVCCM) mkoa wa Mbeya wanatarajia kujibu mapigo leo kwa kuzungumza na waandishi wa habari.

Taarifa za uhakika kutoka ndani ya chama hicho na baadhi ya viongozi wa Jumuiya hiyo zimesema kuwa baada ya baraza hilo kumvua nafasi ya Ukamanda wa UVCCM mkoa wa Mbeya mfanyakazi wa benki kuu ya Tanzania tawi la Mbeya Stephen Mwakajumilo na Mwenyekiti wa Vijana wilaya ya Mbeya mjini Onesmo Nswilla sasa vita kali imeanza.

Imeelezwa kuwa kesho Ijumaa, Mwenyekiti wa UMOJA huo wilaya ya Mbeya mjini Onesmo Nswilla anatarajia kuzungumzia sakata hilo mbele ya waandishi wa habari na kutoa dukuduku lake.

‘’Ni kweli kuna suala hilo litafanyika kesho lakini sijajua ni ukumbi gani na taarifa nilizozipata ni kwamba Nswilla ndiye anayetarajia kuzungumza na vyombo vya habari lakini sijajua upande wa Mwakajumilo kwasababu yeye alinusurika kuvuliwa hata pale Dodoma mwezi January mwaka huu’’ alisema mmoja wa viongozi wa UVCCM mkoa wa Mbeya.

Nswilla alipotafutwa kwa njia ya simu ili kuthibitisha tetesi hizo alikiri kuqwepo kwa mpango huo ambapo alisema kuwa atazungumzia hatima ya uongozi wake na mengine mengi huku akikataa kueleza ni ukumbi gani kutakuwa na mkutano huo kwa madai kuwa atatoa taarifa kwa vyombo vyote baada ya kukamilisha kuupata ukumbi huo.

‘’Ni kweli kesho nitazungumza na vyombo vya habari na na wewe nakuomba uje na nitakujulisha kwa njia ya simu baadae ukumbi ambao nitafanyia na kuelezea masual mbalimbali’’ alisema Nswilla.
 
Taarifa kutoka ndani ya viongozi wa UVCCM mkoa wa Mbeya zimesema kuwa kikao cha baraza la Vijana kikisha azimia jambo si rahisi mamlaka nyingine kuingilia na kutoa maamuzi mbadala zaidi ya yale ya awali.

Wednesday, April 18, 2012

MLINDA MLANGO WA ARSENAL LEO KATIKA HISTORIA





1990
Happy birthday Wojciech Szczesny! Today Wojciech celebrates his 22nd birthday. Send your birthday wishes to him in the comments below:
Wojciech Tomasz Szczęsny (Polish pronunciation: [ˈvɔi̯t​͡ɕɛx ˈʂt​͡ʂɛ̃snɨ]; born 18 April 1990) is a Polish footballer who plays as a goalkeeper for Arsenal and the Poland national team.
His remarkable composure, agility, and command of his area led to his establishment as Arsenal's first choice at just 20 years of age. After winning his place in the first team, Szczęsny expressed his desire of continuing his career as Arsenal's first choice goalkeeper for 15 years.

WANAFUNZI WA SHULE YA ISONGOLE WILAYANI RUNGWE WAFUNGA BARABARA


Wanafunzi wa Shule ya Sekondari Isongole, Wilaya ya Rungwe Mkoani Mbeya wakiwa wameshika mabango yenye ujumbe ulioandikwa "Matuta kwanza tumechoka kupoteza ndugu zetu" kufuatia kifo cha mwanafunzi mwenzao wa kidato cha pili marehemu Nuru Patrick, baada ya kugongwa na gari ya abiria aina ya Coaster na kufariki papo hapo majira ya saa 1 asubuhi, Aprili 17 mwaka huu katika barabara kuu ya Mbeya/Tukuyu.
 Wanafunzi wa Shule ya Sekondari Isongole, Wilaya ya Rungwe Mkoani Mbeya wamelazimika kufunga barabara kuu ya Mbeya/Tukuyu kwa masaa manne kuanzia saa 4 asubuhi mpaka 8 mchana, kufuatia kifo cha mwanafunzi mwenzao wa kidato cha pili marehemu Nuru Patrick, baada ya kugongwa na gari ya abiria aina ya Coaster na kufariki papo hapo majira ya saa 1 asubuhi, Aprili 17 mwaka huu.
 Wanafunzi hao wakiwa wameshika mabango yenye ujumbe ulioandikwa "Matuta kwanza tumechoka kupoteza ndugu zetu" kufuatkia kifo cha mwanafunzi mwenzao wa kidato cha pili marehemu Nuru Patrick, baada ya kugongwa na gari ya abiria aina ya Coaster na kufariki papo hapo majira ya saa 1 asubuhi, Aprili 17 mwaka huu katika barabara kuu ya Mbeya/Tukuyu.
 Mkuu wa Usalama wa barabarani Wilaya ya Rungwe BL Lihwa akimsikiliza Kiranja wa Taaluma katika shule ya Sekondari Isongole Charles Nyingi (26), muda mfupi baada ya ajali kutokea ambapo amesema zaidi ya wanafunzi 15 katika shule za msingi na sekondari Kijijini hapo wamefariki dunia baada ya kugongwa na magari kutokana na mwendokasi hivyo ameomba kuwekwa kivuko na usalama wa barabarani ili kudhibiti mwendokasi wa madereva unaosababisha ajali.
 Mkuu wa Usalama wa Barabarani BL Lihwa akiwasihi wanafunzi kuliachia gari la kusafirishia wagonjwa baada ya kufunga barabara kuu ya Mbeya/Tukuyu kwa masaa manne kuanzia saa 4 asubuhi mpaka 8 mchana, kufuatia kifo cha mwanafunzi mwenzao wa kidato cha pili marehemu Nuru Patrick, baada ya kugongwa na gari ya abiria aina ya Coaster na kufariki papo hapo majira ya saa 1 asubuhi, Aprili 17 mwaka huu.
 Gari la wagonjwa ikiwa imezuiwa kupita baada ya wanafunzi kufunga barabara kuu ya Mbeya/Tukuyu kwa masaa manne kuanzia saa 4 asubuhi mpaka 8 mchana, kufuatia kifo cha mwanafunzi mwenzao wa kidato cha pili marehemu Nuru Patrick, baada ya kugongwa na gari ya abiria aina ya Coaster na kufariki papo hapo majira ya saa 1 asubuhi, Aprili 17 mwaka huu.
 Jeshi la Polisi lililazimika kutumia mabomu ya machozi ili kuwatawanya wanafunzi hao baada ya  kufunga barabara kuu ya Mbeya/Tukuyu kwa masaa manne kuanzia saa 4 asubuhi mpaka 8 mchana, kufuatia kifo cha mwanafunzi mwenzao wa kidato cha pili marehemu Nuru Patrick, baada ya kugongwa na gari ya abiria aina ya Coaster na kufariki papo hapo majira ya saa 1 asubuhi, Aprili 17 mwaka huu.
 Sehemu ya wanafunzi wakiwa na bango lililoamdikwa ujumbe huu "Matuta kwanza tumechoka kuwapoteza ndugu zetu.
Wanafunzi wakiwa wameanza kufunga barabara kuu ya Mbeya/Tukuyu kwa masaa manne kuanzia saa 4 asubuhi mpaka 8 mchana, kufuatia kifo cha mwanafunzi mwenzao wa kidato cha pili marehemu Nuru Patrick, baada ya kugongwa na gari ya abiria aina ya Coaster na kufariki papo hapo majira ya saa 1 asubuhi, Aprili 17 mwaka huu.(Picha zote na Ezekiel Kamanga, Rungwe).

MWANAJESHI AFIKISHWA MAHAKAMANI TENA


ASKARI wa kituo cha jeshi la wananchi Tanzania kikosi cha 44KJ kilichpo katika mji mdogo wa Mbalizi mkoani hapa,Bw.Chacha Mwita pamoja na raia mmoja  aitwaye Bw. Cosmas Maluli jana walipandishwa kizimbani kujibu mashitaka ya kutoa matusi na udhalilishaji  kwa mwenyekiti wa kitongoji  cha Mlima Reli Bw. Ambonisye Ndengelapo Masinga (53).

Ilidaiwa mahakamani hapo na Hakimu wa mahakama ya mwanzo Mbalizi Sofia Fungameza kuwa mnamo tarehe 5 na 7 mwezi huu washitakiwa kwa pamoja walitoa kauli za matusi kwa mwenyekiti huyo pamoja na kamati yake,kwamba walikuwa wamehongwa pesa na kununuliwa pombe ili kutoa maamuzi ya kuwatia hatiani washitakiwa hao.

Hata hivyo, waashitakiwa hao walipotakiwa kutoa hoja kuhusiana na tuhuma zinazo wakabili , walikana kwa maelezo kuwa si kweli.

Hakimu alisema washitakiwa wataendelea kuwa chini ya ulinzi mahakamani hapo hadi watu wa kuwawekea dhamana watakapopatikana.

Kesi hiyo iliahirishwa hadi itakapotajwa tena tarehe 24 mwezi huu kwenye mahakama hiyo,Bw.Mwita amepandishwa kizimbani siku moja baada ya kuvamia moja ya  ofisi za waandishi wa habari jijini hapa na kuwatolea vitisho kwamba atawachukulia hatua kufuatia kuandikwa kwake vibaya kwenye magazeti.

Hivi karibuni mnamo tarehe 7 mwezi huu katika eneo la Tazara Mbalizi askari huyo aliwekwa kitimoto na wananchi wa eneo hilo kwa madai kwamba  amekuwa akiwatishia raia hivyo walimtamkia mbele ya afisa  upelelezi wa mkoa wa Mbeya Bw. Elias Mwita kuwa askari huyo ahame uraiani na kumtaka arudi kambini.

Mkuu huyo wa upelelezi alifika kwenye mkutano huo wa hadhara baada ya kufikishiwa malalamiko ofisini kwake kutoka kwa MchungajiBw. Ayub Mwasiposya,Bw.Cosmas Maluli  na Chacha Mwita ambao walipeleka malalamiko yao ofisi za upelelezi  wakimtuhumu Bw.Mwakilembe kuwa ana wanyanyasa wananchi wa eneo hilo.

Malalmiko hayo yalionekana  hayana ukweli baada ya wananchi waliohudhuria mkutano huo kukanusha madai hayo kwa maelezo kwamba hawana matatizo yoyote na Bw. Mwakilembe huku wakimtaka askari huyo ahame makazi yake mtaani hapo kwa sababu walizo zieleza kuwa ni mchochezi na ana tabia ya kutishia raia.

   

Saturday, April 14, 2012

MADIWANI WA CCM WAGOMA KUJIUNGA NA BIMA YA AFYA CHUNYA

Na Steve Jonas,Mbeya

MADIWANI wa kata 17 kupitia tiketi ya Chama cha Mapinduzi (CCM) wilaya ya Chunya mkoani hapa hivi karibuni wamegoma kujiunga na huduma ya bima ya afya.

Katika hali ya kushangaza kati ya madiwani 42 wa Halmashauri ya Chunya ni madiwani 25 tu walioweza kuwasilisha makablasha yao kwa ajili ya kujiunga na huduma hiyo muhimu kwa jamii wengine  waliobaki wametoa  visingizio mbali mbali vya kuto hitaji huduma hiyo.

Mmoja wa madiwani hao ambaye jina lake halikuweza kufahamika mara moja alidai kuwa huduma hiyo ni muhimu  katika jamii hivyo ilitakiwa madiwani kuwa mstari wa mbele kuwaelimisha wananchi wao  lakini cha kushangaza wao ndio wamekuwa kikwazo cha jamii kuelewa umuhimu wa bima ya afya.

Diwani huyo alisema kitendo cha madiwani kukataa kujiunga na bima ya afya ni kama kukisaliti chama cha CCM ambacho hivi sasa kiko madarakani na kudai kuwa ndicho ki licho buni utaratibu huo ili kuwasaidia wananchi kupunguza gharama za matibabu.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo Mourice Sapanjo alisema chunya imekuwa ikiongozwa na madiwani wa CCM hivyo kitendo cha kukataa kujiunga na huduma hiyo ni kukiuka sera za chama chao.

Alisema kama wengine wanakataa kujiunga ni vyema wakaulizwa ili madiwani wenzao watambue sababu za msingi wanazozitoa vinginevyo aliwataka madiwani hao kufikishwa katika baraza la maadili kwa ajili ya kutoa maelezo yao ya kina kwa kukaidi wito wa serikali.

Katika kikao hicho madiwani hao walitoa changamoto nyingine wakiwatuhumu wabunge wao kwa kutohudhuria vikao vya madiwani ambapo walidai kuwa Mbunge ni diwani hivyo kitendo cha wabunge wa Wilaya ya chunya kutohudhuria vikao ni kinyume na sheria.

Madiwani hao walihoji kuwa iwapo wabunge hawafiki kwenye vikao ambavyo  vina mkusanyiko wa taarifa muhimu za maendeleo na changamoto , wabunge wanapata wapi taarifa za kupeleka bungeni?

Walisema jambo hilo linapaswa kuangaliwa kwa umakini  kwa sababu wabunge wanaweza kupeleka taarifa za uongo bungeni kwa kushindwa kuhudhuriia vikao vya madiwani  kwa maelezo kwambakupita kila kata kuzungumza na wananchi ni jambo ambalo haliwezekani ambapo walipendekeza watumie fursa ya vikao vya madiwani ili kupata changamoto wanazo kabiliana nazo wananchi .

Thursday, April 12, 2012

WANANCHI MBALIZI WAMKATAA AFANDE WA JWTZ KUISHI MTAANI KWAO


 
WANANCHI wa kitongoji cha Mlima Reli cha Mbalizi mkoani hapa wamemtaka askari wa jeshi la wananchi (JWTZ) Chacha Mwita, ahame makazi yake na kurudi kambini kwake kwa kile walichokieleza kwamba askari huyo amekuwa akitishia usalama wa raia.
Hayo yalisemwa jana kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye mtaa wa Tazara katika kitongoji hicho baada ya uongozi kuitisha mkutano huo ili kujadili mahusiano mabaya yaliyokuwepo baina ya askari huyo na raia anaoishi nao mtaani hapo.
Katika mkutano huo alikuwepo mkuu wa upelelezi mkoa wa Mbeya Elias Mwita ambaye alihudhuria baada ya kupokea malalamiko ofisini kwake kwamba hali ya usalama kwa raia wake kwenye eneo hilo haikuwa shwari.
Mkuu huyo aliwaambia wananchi kuwa mapema mwezi huu alipokea ugeni ofisini kwake ulioongozwa na Chacha ukiimtuhumu Benson Mwakilembe kwamba anawanyanyasa wananchi wa eneo hilo.
Alisema Chacha aliongozana na wenzake ambao aliwataja kwa majina kuwa ni Cosmas Maluli na Mchungaji wa kanisa la EAGT usharika wa Galilaya Ayub Mwasiposya ambao wote walikuwa wakimtuhumu Mwakilembe kuwa hana mahusiano mazuri na wananchi wa eneo hilo.
Mwita alisema baada ya kuelezwa hivyo aliona ni vema afike kuwasikiliza wakazi wote wa mtaa huo badala ya kuwasikiliza watu wachache waliofika ofisini kwake.
Mchungaji Mwasiposya aliyekuwa wa kwanza kujieleza katika mkutano huo alikiri kufika ofisini kwa Mwita lakini kwa shinikizo la Chacha aliyemdanganya kwamba wakapatane na Mwakilembe kufuatia tofauti zao  hapo awali.
Mchungaji huyo alikanywa katika mkutano huo kutumia vizuri mahubiri yake ambayo baadhi ya wakazi wamekuwa wakiyalalamikia kwa madai kwamba amekuwa akiipotosha jamii kutokana na kuongelea habari za kishirikina ambazo aliwahi kuzielekeza kwa Mwakilembe.
Sababu zilizopelekea wananchi kumtaka mkuu wa upelelezi amhamishe Chacha kwenye mtaa huo mbali ya vitisho pia walidai kwamba ni mchochezi na hathamini kazi yake kitendo ambacho walikifafanua kuwa analichafua jeshi.
Vilevile wamaeleza amekuwa na tabia ya kuwapeleka watu katika kituo kidogo cha polisi cha Mbalizi bila makosa,amekuwa akizuia sungusungu kufanya kazi yake pia amewahi kuomba rushwa ya sh.100,000 ili kumwachia kijana mmoja ambaye aliyemtuhumu kumwibia kuku wawili madai ambayo walisema hayakuwa ya kweli.
Hata hivyo mkuu huyo wa upelelezi alisema kuwa mtanzania anahaki ya kuishi mahali popote kwa mujibu wa taratibu za serikali lakini pia alifafanua kuwa kwa kuwa Chacha ni mtumishi wa serikali atafanya mawasiliano na viongozi wake ili kuliweka sawa suala la kumtaka Chacha arudi kambini.

Tuhuma hizo zilitolewa katika mkutano huo ambao pia Chacha alipewa fursa ya kujieleza mbele ya mkuu wa upelelezi na alikiri kupeleka malalamiko hayo kwa mkuu huyo wa upelelezi kitendo ambacho kiliibua hasira kwa wananchi na kumtaka asiendelee kujieleza.

Awali Chacha ndiye aliyeuthibitishia mkutano kwa kumtuhumu kijana mmoja ambaye hakumtaja jina kwamba alimkamata akiwa na kuku wawili wa uwizi lakini kauli hiyo ilimgeuka baada ya mama mmoja kusimama na kuueleza umma kuwa, malalamiko ya Chacha kuibiwa kuku  hayakuwa ya kweli kwani aliliunda tukio na kutumia vitisho vya uaskari ili kujipatia kiasi hicho cha pesa.

''Chacha ni mwongo,alimfuata kijana huyo nyumbani kwao na kudai kuwa ameiba kuku wawili wala kuku hao hakukutwa nao ila tunachoamini alichacha na kutumia vitisho hivyo na alifanikiwa kuchukua shilingi laki moja kwa malipo ya hao kuku wawili wa bandia''.Alisema mama huyo katika mkutano wa hadhara

Baada ya mkutano kuisha mwandishi wa habari hizi alipomfuata Chacha kuzungumzia zaidi kuhusu tuhuma hizo hakujibu chochote na wakati huo alionekana kuwa na hasira.

PICHA BILA YA MAELEZO LAKINI UNAWEZA KUHISI


Unaweza ukahisi huyu kama Lulu katika ulinzi na usalama wake
Hizi ni dalili za dharau, nakumbuka mateso ya Bwana Yesu msalabani aliyoyapata kwaajili ya dhambi zetu
Hawa kama wakubwa fulani hivi hapa kwetu Bongo TZ

YURI GAGARIN BINADAM WA KWANZA KUFIKA ANGA ZA MBALI MWAKA 1963



B
inadamu kwa mara ya kwanza alifika katika anga za mbali na kuizunguka dunia.
 
Siku hiyo Yuri Gagarin mwana anga wa Urusi ya zamani aliyekuwa na umri wa miaka 27 aliizunguka dunia kwa dakika 89 kwa kutumia chombo cha anga za mbali kwa jina la Vastok 1 na kwa msingi huyo kulipatikana mafanikio makubwa katika sekta ya masuala ya anga.
Gagarin alifariki dunia akiwa pamoja na mmoja wa viongozi wa ngazi ya juu wa sekta ya masuala ya anga wa Urusi ya zamani katika ajali ya ndege hapo mwaka 1968.

MWIMBAJI WA NYIMBO ZA INJILI APIGWA NONDO


 Mtumishi wa Mungu Bwana Medrick Sanga waimbaji wa Nyimbo za Injili akiwa katika pozi kabla ya kupandishwa jukwaani katika Tamasha la Nyimbo za Injili, sambamba na harambee ya kuchangia fedha za ujenzi wa Kituo cha kulelea Wazee, lililoandaliwa na Bomba FM radio 104.0Mhz Aprili 8 mwaka huu (Sikukuu ya Pasaka) katika Uwanja wa Kumbukumbu ya Sokoine Jijini Mbeya na kudhaminiwa na Kampuni ya SBC Tanzania LTD kupitia kinywaji cha Mountain Dew,  Baraka FM, Sweet FM, Generation FM na Rock FM.
 
Habari na Ezekiel Kamanga, Mbeya.
Muimbaji wa Nyimbo za Injili nchini kutoka Mkoani Mbeya Bwana Medrick Sanga, mkazi wa Makongorosi, Wilaya ya Chunya amejeruhiwa vibaya kichwani baada ya kuvamiwa na watu zaidi ya saba na kupingwa nondo.

Tukio hilo limetokea Aprili 10 mwaka huu majira ya saa 1:45 usiku alipokuwa anaelekea katika Studio ya kurekodi muziki ya Mbeya (Mbeya Records), zilizopo ndani ya Kanisa la KKKT Usharika wa Forest ya zamani Jijini Mbeya.

Muimbaji huyo amesema alikutana na kundi la vijana wapatao saba na kumtaka asimame nay eye kuwauliza kulikoni, kisha wakaanza kumshambulia kwa nondo na mapanga ambapo alikimbilia barabarani na kuomba msaada wa pikipiki hadi Hospitali ya Mkoa.

Aidha tukio hilo limemsababishia muimbaji huyo wa Injili kuvuja damu nyingi mdomoni ambapo ameng’oka meno kadhaa kutokana na kipigo na kupora simu na pesa.

Medrick ni miongoni mwa waimbaji walioshiriki katika Tamasha la nyimbo za Injili sambamba na harambee ya kuchangia ujenzi wa fesha za ujenzi wa Kituo cha Kulelea wazee, lililofanyika Aprili 8 mwaka huu katika Uwanja wa Kumbukumbu ya Sokoine lililoandaliwa na Kituo cha kutushia matangazo Bomba FM redio cha mkoani hapa.

Hata hivyo muimbaji huyo ambaye ni kivutio cha mashabiki awapo jukwaani amefanyiwa vipimo vya uchunguzi (X-RAY), ambapo hali yake kwa sasa inaendelea vema.

CRISTIANO AVUNJA REKODI KUFUNGA MAGOLI 40 ULAYA



U
likuwa ni usiku wa kuvunja rekodi kwa Cristiano Ronaldo !!!!!
*Cristiano amekuwa ndio mchezaji wa kwanza katika ligi kubwa nne (ITA, SPA, GER, ENG) Kufunga magoli 40 katika misimu miwili mfululizo.
 *Pia jana usiku Ronaldo aliweka rekodi ya mchezaji wa kwanza kwenye La Liga kuwahi kufunga mabao 20 katika viwanja vya ugenini.
*Pia Ronaldo amekuwa ndio mchezaji wa kwanza kufunga hat tricks saba katika msimu wa La Liga.

Wednesday, April 11, 2012

MCHUNGAJI MWASIPOSYA NA MWAKILEMBE WAZALIWA UPYA



MUNGU ni mwema,ilikuwa vigumu kuamini au kufikiria kwa uwezo wa akili za kibinadamu kwamba ipo siku moja Bw. Benson Mwakilembe na Mchungaji Ayub Mwasiposya watasikana mikono ya kheri na kuketi meza moja wakijadili na kucheka pamoja kwa furaha,hili limewezekana tena kwa kishindo kikubwa.
Uamuzi wa Mchungaji Mwasiposya kumfuata Bw. Mwakilembe nyumbani kwake kuomba msamaha wa tofauti zao zilizokuwepo kwa kipindi kirefu ni uamuzi wa busara ambao unastahili kuigwa miongoni mwa jamii inayo wazunguka na kwingineko kwani jambo hili ni la kiungwana ambalo pia linaweza kuwa somo ndani ya jamii yetu.

Mtandao wetu(JICHO LANGU BLOGU)ni mtandao ambao unaelewa kwa kina msuguano wa watu hawa yaani Mwakilembe na Mwasiposya,lakini si vema kuyaanika yote hadharani hasa ikizingatiwa kwamba msuguano huo kwa sasa utabakia kuwa historia baada ya Mwasiposya kuomba msamaha kwa Mwakilembe.
Kwa moyo safi Mwakilembe ametamka mbele ya wajumbe kwamba amemsamehe Mwasiposya na kuyafuta yote yaliyojiri nyakati zile za awali na msamaha huo ndio unao warudisha tena watu hao katika asili yao ya undugu kama ilivyokuwa zamani kitendo ambacho kimetafsiriwa kama ni hatua ya ‘KUZALIWA UPYA’.

Si vema wadau wa JICHO LANGU BLOGU nikiwaacha kwenye mataa bila ya kuwajulisha kilicho jiri baina ya Mwasiposya na Mwakilembe,nitakudokezeni kwa kifupi ili kupata japo picha ya tukio hili.
Ni zaidi ya miaka 5 iliyopita Mwakilembe na familia yake alikuwa akiabudu kanisani kwa Mwasiposya(kanisa la EAGT lililopo Mbalizi mkoani Mbeya) lakini alilazimika kumhama mchungaji huyo na kuungama kwa mchungaji Thomas pia wa hilo.
Sababu kubwa iliyomfanya Mwakilembe amkibie mchungaji Mwasiposya ni baada ya mchungaji huyo kumtuhumu mke wa mwakilembe,Andwele Mwakilembe kwamba ni ajenti wa kuzimu.Tangu hapo mawasiliano ya watu hawa yakawa si ya kawaida kwa maana kwamba chuki iliibuka baina yao.

Baada ya muda mrefu kuishi katika mazingira hayo, mwaka jana liliibuka zengwe linguine.Hili pia lilikuwa dongo zito alilotupiwa Mwakilembe ambaye maombi yake yalipokelewa vyema na mwenyezi mungu na kumnyooshea mfereji wa pesa katika biashara zake wakati akiwa amesota ‘MAKAVU’ kwa miaka dahari iliyopita.
Kama ilivyokuwa awali ,mchungaji huyo alisikika kwenye vipaza sauti akiporomosha vipande vya maneno ya kebehi ikiwa ni pamoja na kuutangazia umma kwamba Mwakilembe anamiliki mali za kuzimu,hili ndilo tatizo kubwa liliosababisha mchungaji huyo kutupwa mikononi mwa polisi na bifu liliendelea la chini chini yaani Zali baridi.

Lakini sasa wamefikia hatua wamepatana na kuziweka kando tofauti zao,upatanisho huoulifanyika chini ya wajumbe 11nyumbani kwa Mwakilembe mnamo tarehe 7 Aprili,2012 na siku iliyofuata ya Pasaka Mwakilembe alikaribishwa kanisani kwa Mwasiposya ambako alihudhuria Ibasda ya pasaka kasha Mwasiposya kutangazia waumini kwamba yeye na Mwakilembe ni ndugu hawana tena tofauti zao.

SWALI; Je Mwakilembe atarudi tena kundini kwa Mwasiposya au ataendelea kwa Mchungaji Thomas?

Friday, April 6, 2012

MCHUNGAJI AZOMEWA KWENYE MKUTANO WA HADHARA


MCHUNGAJI wa kanisa la Evangelist Asesemblies of God Tanzania usharika wa Galilaya Mbalizi jijini Mbeya, Ayub Mwasiposya jana alijikuta katika wakati mgumu baada ya kuzomewa na wananchi katika mkutano wa hadhara. 
 
Mchungaji huyo alipata aibu ya kuzomewa na wananchi waliohudhuria mkutano huo uliofanyika eneo la Tazara katika mji mdogo wa Mbalizi baada ya kupata nafasi ya kujieleza ni kuhusu taarifa alizo shiriki kuzipeleka kwenye ofisi ya  mkuu wa upelelezi mkoa wa Mbeya.
 
Habari zinasema kuwa, mchungaji huyo pamoja na wenzake wawili alipeleka malalamiko kuwa wananchi wa mtaa wa Tazara wananyanyaswa na mfanyabiashara aliyetajwa kwa jina la Benson Mwakilembe na kudai kuwa wananchi hao wamefikia hatua kumtaka Mwakilembe ahame katika mtaa huo.  
 
  Habari zaidi kuhusiana na tukio hilo zinasema kwamba mchungaji huyo aliwaongoza wenzake kwa shinikizo la uchochezi wengine  waliotajwa ni majina ya Cosmas Maluli na Chacha Mwita hadi kwenye ofisi za upelelezi mkoani na kueleza malalamiko hayo .   
 
Taarifa kutoka ndani ya jeshi la Polisi mkoani hapa zinasema kuwa baada ya kupata taarifa hizo waliwasiliana na uongozi wa mtaa  uongozi ambao ulikana kuwepo na tuhuma hizo na ulipendekeza ufanyike mkutano wa hadhara ili kuthibitisha tuhuma hizo mbele ya wananchi.
  
Katika mkutano huo ambao ulianza majira ya saa 11 za jioni ukihudhuriwa na mkuu wa kituo  kidogo cha Polisi kilichopo Mbalizi ,Seleman Manyanga, viongozi wa serikali ya mtaa huo na wananchi wa eneo hilo ulishindwa kufikia muafaka baada ya RCO kushindwa kufika.
  Baadhi ya watu waliohojiwa na mwandishi wa habari hizi eneo la Tazara Mbalizi wamesema kuwa, chanzo cha mchungaji huyo kuzomewa kilitokana na yeye kujiingiza kwenye ugomvi na mfanyabiashara huyo kwa kipindi kirefu huku akimtuhumu Mwakilembe kujipatia mali kwa njia za kishirikina.
"Hakuna lolote ni wivu tu unao wasumbua baada ya mwenzao kubahatika kupata mali ambazo tunafahamu kazisotea kwa muda mrefu huko machimboni,"aliyasema mmoja wa wananchi aliyejitambulisha kwa jina moja la Sanga .
   Mwasiposya mnamo mwaka jana aliingia kwenye ugomvi mkubwa na Mwakilembe ambaye pia aliwa kuwa muumini wake, ugomvi huo ulimfikisha Mwasiposya Mikononi mwa polisi yeye na familia yake iliyofika kituo cha polisi Mbalizi na kufanya fujo muda mfupi baada ya Mwasiposya kukamatwa.
  Akiwa mikononi mwa polisi ,Mwasiposya alifuatwa na watoto wake kwa kusudi la kujua kosa la baba yao hatimaye nao wakajikuta wako hatiani kama ilivyo kuwa kwa baba yao kufuatia vurugu zao.
 
  Vile vile mchungaji huyo amelalamikiwa na baadhi ya wakazi wa vitongoji vya Chapakazi naMlimareli kwa madai kuwa mahubiri yake yamekuwa kero kwa wakazi hao kutokana na mchungaji huyo kuhubiri kwa sauti kubwa ya vipaza sauti usiku wa manane.
Akizungumza na mwandishi wahabarihizi nyumbani kwake mwenyekiti wamtaa wa Chapakazi aliyejitambulishakwa jinala Jacob Ntengule alikiri kupokea malalamiko hayo kutoka kwa wakazi wamtaa wake .
Ntengule alisema kwamba ,mahubirihayo yamekuwayakiharibu doria inayo fanywa  na sungu sungu wamaeneo hayo.
  
   Mchungaji Mwasiposya alipofuatwa nyumbani kwake ilikuelezea tukio hilo  alikiri pamoja na kupokea onyo la kuhubiri usiku wa manane.
    Balozi wa mtaa wa Chapakazi ameshauri kuwa serikali iingilie kati suala hilo kwa madai kuwa kunadalili mbaya ya uvunjifu wa amani.
 Mwakilembe alipohojiwa na mwandishi wa habari hizi alisema kuwa amedhalilishwa sana na mchungaji wake na kudai kuwa ameishangaza jamii inayo mzunguka kwa udhaifu wa kiimani.

Wednesday, April 4, 2012

MEYA WA JIJI LA MBEYA ATEKWA NA MAJAMBAZI MBARALI.

TAARIFA zilizotufikia ni kwamba Meya wa Jiji la Mbeya Athanas Kapunga pamoja na msafara wa madiwani waliokuwa wametoka mkoani Morogoro kwa ajili ya kuishangilia timu ya Jiji hilo jana majira ya saa tano usiku alitekwa na majambazi eneo wilaya ya Mbarali mkoani Mbeya.

Taarifa zaidi zaja, huku madiwani wakikosa imani na Kamanda wa Jeshi la Polisi mkoani humo Advocate Nyombi..

WALIMU MBEYA WASHINIKIZA KIONGOZI WAO ARUDISHWE MADARAKANI

 
ZAIDI ya walimu 50 wa Halmashauri ya wilaya ya Mbeya juzi waliandamana katika ofisi za Chama cha Walimu wilaya ya Mbeya(CWT) wakishinikiza kurejeshwa kazini kwa aliyekuwa Mwenyekiti wa chama hicho ambaye alisimamishwa na kamati tendaji ya wilaya hiyo.
 
Walimu hao wameliambia gazeti hili kuwa kamati hiyo haikumtendea haki mwenyekiti wao waliyemtaja kwa jina la Anthony Mwaselela ambaye aliandikiwa barua ya kusimamishwa na uongozi mnamo Januari 16, mwaka huu ambayo ilisainiwa na katibu wa CWT wilaya ya Mbeya Monica Haule.
 
Kwa mujibu wa barua hiyo( nakala zake tunazo), mwenyekiti huyo anatuhumiwa kushiriki vikao vya walimu waliojiendeleza kielimu ambao wanafahamika kama  Umoja wa maafisa Elimu Tanzania(UMET).
 
Awali walimu hao waliwahi kufunga ofisi za CWT Mkoa na ofisi ya  Mbeya vijijini kwa madai kwamba, katibu wa CWT Mkoa alishindwa kuwaandikia barua ya kuwaruhusu kwenda Ikulu  kumwona Rais kwa kusudi la kupinga waraka kandamizi uliokuwa umetolewa dhidi yao.
Aidha,katibu hyo pia anatuhumiwa  kutoshirikiana na viongozi wenzie  kwenda polisi kushughulikia kufunguliwa kwa ofisi za CWT  kitendo ambacho inadaiwa ni kukiuka  katiba ya chama hicho ibara ya 41(iv) na (v).

Ukiukwaji huo wanasema ulisababisha wanachama kukosa huduma za kiofisi,kushindwa kuangalia usalama wa mali za chama na kukosa mawasiliano kati ya wilaya moja hadi nyingine.
 

 
 Kwa mujibu wa barua walioandikiwa wawakilishi wa shule  wa halmashauri hiyo yenye kumbukumbu namba CWT/MBV/WAW/11/01 kutokana na makosa  ,kamati ya utendaji ya wilaya ilifikia maamuzi ya kumsimamisha uongozi mwenyekiti huyo hadi utakapofanyika mkutano mkuu ambao utakuwa na maamuzi ya kumuondoa au kumrudisha kwenye madaraka hayo.
 
Hata hivyo, walimu hao walidai kuwa hawakushirikishwa katika maamuzi hayo kitendo ambacho walisema ni cha kibabe kwani hata barua aliyoandikiwa Mwaselela iliwafikia wanachama wachache tena kwa siri.
 
Walifafanua kwamba, wenye maamuzi ya kumvua madaraka kiongozi wa kuchaguliwa ni wanachama wenyewe kupitia mkutano mkuu  kwa mujibu wa katiba ya chama hicho na kudai kuwa kamati tendaji ilikiuka kanuni za chama hivyo walitaka mwenyekiti huyo arudishwe madarakani huku mkutano mkuu ukisubiliwa.
 
Maandamano ya walimu hao kwenye ofisi za CWT Wilaya ya Mbeya zilizopo uwanja wa Sokoine jijini hapa hayakufanikiwa kuwakuta viongozi wao hali iliyopelekea mwenyekiti wa CWT mkoa wa Mbeya Nelusigwe Kayuni na katibu wake Kasuku Bilago kulazimika kukaa kukaa na kujadili na walimu hao.
 
Kayuni alitumia muda mrefu kuwafafanulia walimu hao katiba ya chama na taratibu walizopaswa kuzifuata ingawa naye alikri kuwa kamati tendaji haikumtendea haki mwenyekiti huyo huku akieleza kuwa ofisi ya CWT mkoa hawana uwezo wa kutengua uamuzi huo bali walitakiwa wasubiri mkutano mkuu kwa ajili ya maamuzi.
 
Hali ilizidi kuwa tete baada ya mwenyekiti wa mkoa  kuwaambia kuwa mwaka huu hakutakuwa na mkutano mkuu wa chama hicho nchi nzima bali kwa dharula mkutano huo utakuwepo kwaajili ya tuhuma hizo pekee na kuwataka walimu hao kuwa wavumilivu.
 
Katika mkutano huo mvutano ulikuwa mkali kati ya uongozi wa CWT mkoa na walimu hao hali iliyowapelekea baadhi ya walimu kuanza kutawanyika mmoja baada ya mwingine kwa madai kuwa hawakuridhishwa na majibu ya viongozi hao na baadhi ya walimu hao walitishia kuzifunga tena ofisi hizo.