Monday, April 23, 2012

MBEYA CITY YAWASONONSHA MASHABIKI WA SOKA MBEYA


TIMU ya  Mbeya City ya mkoani hapa  imewasonesha mashabiki  wa soka jijini hapa  baada ya kupokea kichapo cha mabao 2-0 kutoka kwa  timu ya Polisi Morogoro kwenye  mchezo uliochezwa mjini Morogoro,na  kufuta ndoto za kucheza Ligi kuu msimu ujao.

 Mashabiki walioongea  na majira mjini hapa  kwa nyakati tofauti  wamesema  kuwa  kushindwa kupanda daraja kwa timu hiyo ,kumechangiwa na kocha mkuu wa timu hiyo Juma Mwambusi  baada ya kuachiwa madaraka yote ya timu na kujiamini kupita kiasi.

Shabiki  wa soka jijini hapa  Lugano Hezron   alisema kuwa timu hiyo ya Halmashauri ya jiji la Mbeya ,ilkuwa na uwezo wa kupanda daraja kutokana na kusheheni wachezaji wenye vipaji lakini uongozi ndio ulioboronga .

Aliwataja wachezaji hao kuwa ni Venance Muligo,Josephat Maston ambao wana uwezo mkubwa  kiuchezaji lakini waliachwa dakika za mwisho kutokana na sababu zisizojulikana,ambapo nahodha wa timu hiyo Patrick Mangungulu alifukuzwa kambini mjini Morogoro kutokana na utovu wa nidhamu.

Wachezaji wengine ni  Fidel Castro,mlinda mlango Aswile Asukile, Moses Mwazembe,David Mpangala pamoja na wachezaji  ambao ni nguzo kubwa ya timu hiyo,lakini hawakutumiwa vizuri na hivyo kuwakosesha  mashabiki wa Mbeya uhondo wa kuiona ligi kuu kama walivyotegemea kuwa  na timu mbili  za mkoa wa Mbeya City na Prisons zote za jijini hapa.

Mdau mwingine wa soka aliyejitambulisha kwa jina la Shomari Rajabu  alisema kuwa sababu kubwa iliyofanya City wasipande daraja,ni kwamba mwalimu wa timu hiyo  Mwambusi hakuwa na benchi la ufundi lenye uwezo wa kumshauri pale timu hiyo inapo shinda au kufungwa.

Aliongeza kwamba timu hiyo ilkuwa na uwezo mkubwa wa kifedha kiasi kwamba wangeongeza nguvu kwenye benchi  la  ufundi ,ila wakaridhika na uwezo wa kocha mkuu pekee kwa vile timu ilikuwa inashinda .

Mdau huyo  ametoa ushauri kwa timu hiyo kwamba mwakani wakifanikiwa kuingia kwenye hatua  za fainali za ligi daraja la kwanza ,waongeze nguvu katika benchi la ufundi ili washirikiane mwalimu wa timu hiyo.

Shabiki  Geofrey Kilumbi alisema kuwa kushindwa kupanda daraja kwa Mbeya City na kuikosa Ligi kuu msimu ujao,kulitokana na kujiamini kupita kiasi kwa timu hiyo.

Akifafanua zaidi  alisema kuwa hatua hiyo ilitokana na timu hiyo kushinda karibu mechi zote za hatua ya awali ilizocheza za nyumbani na ugenini.
Mwambusi akizungumza kwa njia ya simu kutoka mkoani Morogoro ambako mashinda hayo ya tisa bora yalifanyika , alisema kushindwa kwa Mbeya City kufuzu, kumetokana na wao kukosa uzoefu wa mashindano ya kituo na sio Ligi.
MWISHO

No comments:

Post a Comment