TUKIO la mwalimu wa shule ya msingi ya Juhudi ya jijini
hapa kufukuzwa shuleni hapo akituhumiwa
kujihusisha na vitendo vya ushikina mapema mwezi Aprili mwaka huu ,limechukua
sura mpya baada ya kubainika baadhi ya wanafunzi pia kujihusisha na vitendo
hivyo.
Hayo yalisemwa katika mkutano wa hadhara uliofanyika mnamo
Aprili 19 mwaka huu mkutano ambao ulikusudia kuzungumzia mapato na matumizi ya
shule hiyo baada ya kutokea mtafaruku kati ya wazazi na kamati ya shule.
Katika mkutano huo, mwenyekiti wa mtaa wa Mwambenja Bw.Lucas
Mwakalonge alisema kuwa wanafunzi watatu walikamatwa na walinzi shuleni hapo
wakiwa katika harakati za vitendo vya kishirikina.
Bw.Mwakalonge alisema kwamba baada ya wananchi kukusanyika
na kujionea tukio hilo waliamuru watoto hao wafikishwe mikononi mwa Polisi ili
wakatoe maelezo ambako waliachiwa kwa dhamana baada ya kutoa maelezo.
Baada ya kugundua kwamba wanafunzi hao walikuwa wakijihusisha na vitendo vya
kishirikina baadhi ya wazazi waliamua kumuomba msamaha mwalimu aliyetajwa kwa
jina moja la Kyando ambaye awali alituhumiwa kuhusika na vitendo hivyo kasha
kumfukuza shuleni hapo.
Hata hivyo,baadhi ya wananchi bado walionesha dalili za
kutokubaliana na suala la kumuomba radhi mwalimu huyo kwa kukosa imani naye.
Mwenyekiti huyo alisema matukio kama hayo si mageni katika
mtaa huo kitendo ambacho kimekuwa kikieneza sifa mbaya ya mtaa wa
Mwambenja,tukio hilo na lile lililo sababisha mwalimu Kyando kuondolewa shuleni
hapo ni sawa na tukio lililo wahi kutokea miaka 15 iliyopita.
Mapema mwezi huu kando kando ya mto jirani na shule
vilikutwa vitu vya ajabu ambavyo vilisadikika kuwa ni vitu vya kishirikina,vitu
hivyo ni Vibuyu,vyungu viwili,fuvu la kichwa cha ng’ombe,pembe moja la ng’ombe
na vitambaa viwili vyenye rangi nyeusi na nyekundu ambavyo vilifungwa kwenye
miti miwili tofauti.
Mmoja wa wajumbe waliohudhuria mkutano huo aliyefahamika kwa
jina la Frank Jacob,bila ya kufafanua aliwataka walimu wote wa shule ya Juhudi
pamoja na kamati ya shule wakae na kumaliza tofauti zao ambazo zimekuwa
zikitapakaza sifa mbaya ndani ya jamii inayo wazunguka.
No comments:
Post a Comment