K
|
ocha Mkuu wa Taifa
Stars, Kim Poulsen leo (Mei 14 mwaka huu) ametangaza kikosi cha wachezaji 25
kwa ajili ya mechi ya mchujo ya Kombe la Dunia hatua ya makundi Kanda ya Afrika
dhidi ya Ivory Coast.
Akitangaza
kikosi hicho ambacho kitaingia kambini kesho kutwa (Mei 16 mwaka huu, Kim
amesema uteuzi wake umezingatia uwezo wa mchezaji uwanjani, nafasi anayocheza
na ubora wake.
Wachezaji
walioitwa ni makipa; Juma Kaseja (Simba), Mwadini Ally (Azam) na Deogratius Munishi
(Mtibwa Sugar). Mabeki ni Nassor Masoud Cholo (Simba), Aggrey Morris (Azam),
Amir Maftah (Simba), Erasto Nyoni (Azam), Kelvin Yondani (Simba), Waziri Salum
(Azam), Shomari Kapombe (Simba) na Juma Nyoso (Simba).
Viungo
ni Mwinyi Kazimoto (Simba), Salum Abubakar (Azam), Nurdin Bakari (Yanga), Jonas
Mkude (Simba), Shabani Nditi (Mtibwa Sugar), Edward Christopher (Simba- U20),
Mrisho Ngasa (Azam) na Frank Domayo (JKT Ruvu- U20).
Washambuliaji
ni Mbwana Samata (TP Mazembe, Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo), Ramadhan
Singano (Simba-U20), Simon Msuva (Moro United- U20), Thomas Ulimwengu (TP
Mazembe, Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo), Haruna Moshi (Simba) na John Bocco
(Azam).
Stars
inayodhaminiwa na Kampuni ya Bia Tanzania (TBL) kupitia bia ya Kilimanjaro
itacheza mechi ya kirafiki nyumbani Mei 26 mwaka huu dhidi ya Malawi kabla
kuivaa Ivory Coast ugenini Juni 2 mwaka huu jijini Abidjan.
No comments:
Post a Comment