KESHO WATAKUWA WAKIUAGA MWILI WA MAREHEMU KATIKA VIWANJA VYA
LEADERS CLUB JIJINI DAR ES SALAAM NA KUUSAFIRISHA KWENDA DRC KWANI YEYE
NI MRWANDA MWENYE ASILI YA KONGO.
Shirikisho la Mpira wa
Miguu Tanzania (TFF) limepokea kwa masikitiko kifo cha mchezaji wa Simba na
timu ya Taifa ya Rwanda (Amavubi), Patrick Mafisango kilichotokea leo alfajiri
(Mei 17 mwaka huu) kwa ajali ya gari Dar es Salaam.

Msiba
huo ni mkubwa kwa familia ya mpira wa miguu kwani Mafisango kwa kipindi chote
alichocheza mpira hapa nchini akiwa na timu za Azam na baadaye Simba, aliifanya
kazi yake (kucheza mpira) kwa bidii.
Kifo
chake ni pigo kubwa si tu kwa familia yake na timu alizochezea, bali ukanda
mzima wa Afrika Mashariki na Kati ambapo changamoto zake zilikuwa dhahiri
uwanjani.
Wakati
mauti inamkuta, Mafisango alikuwa ameitwa Amavubi kwa ajili ya mechi za mchujo
za Kombe la Dunia, Kanda ya Afrika zinazochezwa mapema mwezi ujao.
TFF
inatoa pole kwa familia ya Mafisango, klabu ya Simba, Shirikisho la Mpira wa
Miguu Rwanda (FERWAFA) na kuwataka kuwa na subira na uvumilivu katika kipindi
hiki kigumu cha msiba huo mzito.
Mungu
aiweke roho ya marehemu Mafisango mahali pema peponi. Amina
No comments:
Post a Comment