Mwanafunzi wa Kidato cha Pili katika
Shule ya Sekondari Isange ,mkazi wa Isanu, Kata ya Isange, Wilaya ya
Rungwe Mkoani Mbeya mnamo Mei 11 mwaka huu amefariki dunia baada ya kujinyonga kwa kutumia kamba ya
kufungia ng'ombe muda mfupi baada ya kugundua alikuwa na ujauzito wa miezi mitatu .
Afisa mtendaji wa Kata hiyo Bwana
Anyambege Mwangomo amelitaja jina la marehemu kuwa ni Enitha Ndambo
(15), ambaye alikuwa akiishi na bibi yake Bi Emelia Ndenga.
Marehemu alichukua hatua ya kujinyonga wakati mlezi wake akiwa katika kilabu cha pombe na kamba
aliyotumia ilikuwa ndani ya nyumba hiyo waliyokuwa wakiishi.
Polisi walifika kwenye eneo la tukio na kuuchukua mwili wa marehemu na
kuupeleka katika Zahanati ya Isange kwa ajili ya kufanya upasuaji, ili
kuthibitisha kama alikuwa na ujauzito na mara baada ya upasuaji
waliwaruhusu wanakijiji kuzika mwili wa marehemu na kiumbe
kilichokuwa tumboni.
Mwili
wa marehemu ulifanyiwa uchunguzi na Daktari Kalinga kutoka katika
Hospitali ya Serikali ya Makandana iliyopo wilayani humo, na zoezi la
upimaji wa mimba wanafunzi ulifanywa na Daktari Anna Mwelevu wa Zahanati ya
Isange..
Aidha katika uchunguzi uliofanywa
umebaini aliyemsababishia ujauzito ni mwanafunzi wa shule hiyo Alex
Mwaitege, anayesoma kidato cha kwanza.
No comments:
Post a Comment