Monday, May 21, 2012

KANISA LA UINJILISTI NA MKAKATI WA MAENDELEO YA JAMII


Mchungaji Markus Lehner (kushoto) akiwa kwenye moja ya kazi za Kanisa la Uinjilist Mbalizi mkoani Mbeya

 Steve Jonas,Mbeya


Na kila jambo linaumuhimu wake kwenye nafasi yake kulingana na mazingira husika kwa mujibu wa jiografia ya eneo analoishi binadamu wa leo.

Zipo changamoto nyingi anazokabiliana nazo mwanadamu katika maisha yake ya kila siku ,pia changamoto hizi zimebeba uzito mkubwa ambao ambao umekuwa kero katika uboreshaji wa huduma za kijamii.

Ni wazi kwamba jamii inahitaji kupata huduma zilizo bora kwa wakati muafaka ambapo matokeo ya huduma bora  ni kuwa na jamii yenye ufahamu mzuri,uelewa wa mambo mbali mbali na ubunifu.

Matokeo haya ni chanzo cha kuwa na taifa lenye watu makini katika kukuza kipato cha kukidhi mahitaji yao ya kila siku na kupanua wigo wa pato la taifa.

Lakini kikubwa zaidi katika hili ni kuunda msingi mzuri  kwa kuiandaa jamii ili iweze kufika pale panapokusudiwa,haijalishi ni mazingira gani bali mawazo endelevu na chanya katika maarifa yanayoweza kuikwamua jamii kwenye hali ya umasikini.

Yapo mambo mengi niniyoweza kuyaelezea kwa upana zaidi kuhusiana na kero zinazo izunguka jamii ya kitanzania,lakini leo ni vyema nielekeze nguvu zangu kwa kile kilichonisukuma kuandika makala haya.

Fikra na uelewa wangu ni vitu viwili ambavyo vimezama ndani ya shughuli zinazo fanywa na kanisa la Uinjilisti Tanzania lililopo Mbalizi katika Halmashauri ya Wilaya ya Mbeya.

Kanisa hilo limewekeza nguvu kubwa kuikwamua jamii kimaendeleo na kupunguza hali ngumu ya maisha anayokabiliana nayo mtanzania wa kipato cha chini.

Mchango wa kanisa hilo umejidhihirisha kwenye mikoa ya nyanda za juu kusini ambayo ni Iringa,Mbeya,Njombe,Ruvuma,Rukwa na Katavi.

Mkurugenzi wa kanisa hilo ,Mchungaji Markus Lehner  ofisini kwake jijini Mbeya alisema kuwa mbali ya kanisa kuhubiri neno la Mungu pia linahudumia jamii  kukuza elimu kwa kusaidia ujenzi wa shule za msingi na sekondari.

 Huduma zingine   ni za afya kwa ujenzi wa vituo vya afya na  hospitali teule ya Wilaya ya Mbeya na kuwapatia ujuzivijana kwa kujenga vyuo vya ufundi katika mikoa hiyo ya kanda ya nyanda za juu kusini.

Alisema  wananchi walikuwa wakitaabika kupata huduma hizo na kulazimika kusafiri umbali wa zaidi ya kilomita 10 ambapo tatizo hilo kwa sasa limepungua baada ya kukamilika  hospitali hiyo ambayo kwa mujibu wa mganga mkuu hospitalini hapo,Bw.Msafiri Kimaro, ina uwezo wa kulaza wagonjwa 200 kwa wakati mmoja.

Hospitali hiyo ilizinduliwa Oktoba 18 mwaka 2008 na Rais,Jakaya Kikwete ni tegemeo  kwa wananchi mkoani humo na  mikoa jirani huku ikipunguza msongamano wa wagonjwa kwenye hospitali zingine kama ilivyokuwa hapo awali.

Bw.Lehner alisema ili kukabiliana na tatizo la kukatika kwa umeme kanisa lilifanikiwa kupata wafadhiri kutika shirika lisilo la kiserikali kutoka Uswis na kuiwezesha Hospitali  kupata umeme wa jua uliogharimu zaidi ya shilingi milioni 200.

Alisema umeme huo utatoa huduma za hospitali kama vile upasuaji na wadi ya uzalishaji ambapo alithibitisha kuwa utadumu kwa muda wa zaidi ya miaka 30.

Hata hivyo, mchungaji Lehner alisema zipo changamoto ambazo zinahitaji mkono wa serikali ambazo ni maji na vyombo vya usafiri kwa watumishi wa hospitali.

Mchungaji Lehner alishauri madhehebu kubuni mbinu kujipatia kipato kitakacho jenga uchumi wa jamii badala ya kutegemea sadaka za waumini.

Pia kanisa linashughulika na kuhifadhi mazingira, kituo cha kutolea elimu kuhusu mazingira na utamaduni wa maisha ya watu wa kale na hifadhi ndogo ya wanyama kama ishara ya urithi kutoka kwa watu wa kale.

Baadhi ya wananchi waliohojiwa na gazeti hili wakazi wa vijiji jirani na hospitali hiyo walisema kuwa ,tangu Tanzania ilipopata uhuru wake mwaka 1961 hawakuwahi kupata huduma ya maji ya bomba ambayo kwa sasa wananufaika kupitia huduma za hospitali hiyo.

 0762 876 892

3 comments:

  1. amen mungu awabariki sana by katibu wa kanisa tawi la tabora Victor Nalibwini oredi

    ReplyDelete
  2. Hiyo imekaa vizuri. Naomba kupata mawasiliano ya viongozi wa kanisa hili tafadhali. Kuna mambo natamani kuyajua kutoka kwao. Unaweza kunitumia kwa na 0767422383

    ReplyDelete