Mchungaji Markus Lehner (kushoto) akiwa kwenye moja ya kazi za Kanisa la Uinjilist Mbalizi mkoani Mbeya |
Steve Jonas,Mbeya
Na
kila jambo linaumuhimu wake kwenye nafasi yake kulingana na mazingira husika
kwa mujibu wa jiografia ya eneo analoishi binadamu wa leo.
Zipo
changamoto nyingi anazokabiliana nazo mwanadamu katika maisha yake ya kila siku
,pia changamoto hizi zimebeba uzito mkubwa ambao ambao umekuwa kero katika
uboreshaji wa huduma za kijamii.
Ni
wazi kwamba jamii inahitaji kupata huduma zilizo bora kwa wakati muafaka ambapo
matokeo ya huduma bora ni kuwa na jamii
yenye ufahamu mzuri,uelewa wa mambo mbali mbali na ubunifu.
Matokeo
haya ni chanzo cha kuwa na taifa lenye watu makini katika kukuza kipato cha
kukidhi mahitaji yao ya kila siku na kupanua wigo wa pato la taifa.
Lakini
kikubwa zaidi katika hili ni kuunda msingi mzuri kwa kuiandaa jamii ili iweze kufika pale
panapokusudiwa,haijalishi ni mazingira gani bali mawazo endelevu na chanya
katika maarifa yanayoweza kuikwamua jamii kwenye hali ya umasikini.
Yapo
mambo mengi niniyoweza kuyaelezea kwa upana zaidi kuhusiana na kero zinazo
izunguka jamii ya kitanzania,lakini leo ni vyema nielekeze nguvu zangu kwa kile
kilichonisukuma kuandika makala haya.
Fikra
na uelewa wangu ni vitu viwili ambavyo vimezama ndani ya shughuli zinazo fanywa
na kanisa la Uinjilisti Tanzania lililopo Mbalizi katika Halmashauri ya Wilaya
ya Mbeya.
Kanisa
hilo limewekeza nguvu kubwa kuikwamua jamii kimaendeleo na kupunguza hali ngumu
ya maisha anayokabiliana nayo mtanzania wa kipato cha chini.
Mchango
wa kanisa hilo umejidhihirisha kwenye mikoa ya nyanda za juu kusini ambayo ni
Iringa,Mbeya,Njombe,Ruvuma,Rukwa na Katavi.
Mkurugenzi
wa kanisa hilo ,Mchungaji Markus Lehner ofisini
kwake jijini Mbeya alisema kuwa mbali ya kanisa kuhubiri neno la Mungu pia
linahudumia jamii kukuza elimu kwa
kusaidia ujenzi wa shule za msingi na sekondari.
Huduma zingine
ni za afya kwa ujenzi wa vituo vya
afya na hospitali teule ya Wilaya ya
Mbeya na kuwapatia ujuzivijana kwa kujenga vyuo vya ufundi katika mikoa hiyo ya
kanda ya nyanda za juu kusini.
Alisema
wananchi walikuwa wakitaabika kupata
huduma hizo na kulazimika kusafiri umbali wa zaidi ya kilomita 10 ambapo tatizo
hilo kwa sasa limepungua baada ya kukamilika hospitali hiyo ambayo kwa mujibu wa mganga
mkuu hospitalini hapo,Bw.Msafiri Kimaro, ina uwezo wa kulaza wagonjwa 200 kwa
wakati mmoja.
Hospitali
hiyo ilizinduliwa Oktoba 18 mwaka 2008 na Rais,Jakaya Kikwete ni tegemeo kwa wananchi mkoani humo na mikoa jirani huku ikipunguza msongamano wa
wagonjwa kwenye hospitali zingine kama ilivyokuwa hapo awali.
Bw.Lehner
alisema ili kukabiliana na tatizo la kukatika kwa umeme kanisa lilifanikiwa
kupata wafadhiri kutika shirika lisilo la kiserikali kutoka Uswis na kuiwezesha
Hospitali kupata umeme wa jua
uliogharimu zaidi ya shilingi milioni 200.
Alisema
umeme huo utatoa huduma za hospitali kama vile upasuaji na wadi ya uzalishaji
ambapo alithibitisha kuwa utadumu kwa muda wa zaidi ya miaka 30.
Hata
hivyo, mchungaji Lehner alisema zipo changamoto ambazo zinahitaji mkono wa
serikali ambazo ni maji na vyombo vya usafiri kwa watumishi wa hospitali.
Mchungaji
Lehner alishauri madhehebu kubuni mbinu kujipatia kipato kitakacho jenga uchumi
wa jamii badala ya kutegemea sadaka za waumini.
Pia
kanisa linashughulika na kuhifadhi mazingira, kituo cha kutolea elimu kuhusu
mazingira na utamaduni wa maisha ya watu wa kale na hifadhi ndogo ya wanyama
kama ishara ya urithi kutoka kwa watu wa kale.
Baadhi
ya wananchi waliohojiwa na gazeti hili wakazi wa vijiji jirani na
hospitali hiyo walisema kuwa ,tangu Tanzania ilipopata uhuru wake mwaka
1961 hawakuwahi kupata huduma ya maji ya bomba ambayo kwa sasa
wananufaika kupitia huduma za hospitali hiyo.
amen mungu awabariki sana by katibu wa kanisa tawi la tabora Victor Nalibwini oredi
ReplyDeleteUbarikiwe piah
ReplyDeleteHiyo imekaa vizuri. Naomba kupata mawasiliano ya viongozi wa kanisa hili tafadhali. Kuna mambo natamani kuyajua kutoka kwao. Unaweza kunitumia kwa na 0767422383
ReplyDelete