Wednesday, March 14, 2012

MAHAKAMA YA KIMATAIFA (ICC) YATOA HUKUMU KWA LUBANGA





 
 
 

 
 
 

 
 
 


M
ahakama  ya  kimataifa  inayohukumu  kesi  za  uhalifu wa  kivita  mjini  The  Hague imempata   na  hatia   ya uhalifu  wa  kivita Thomas  Lubanga  Dyilo , katika  hukumu yake  ya  kwanza  ya  kihistoria   tangu  mahakama  hiyo iundwe muongo  mmoja  uliopita. 
JICHO LANGU BLOGU NA MARTUKIO
Lubanga  ameshutumiwa  kwa  kuwaingiza  na  kuwatumia vijana  wadogo   katika   jeshi  wakati  wa  miaka  mitano  ya mzozo  wa  kivita  katika  jamhuri  ya  kidemokrasi  ya Congo uliomalizika  mwaka  2003. 
Watu  wanaokadiriwa kufikia  60,000  wameuawa  katika  mzozo  huo.  Mcheza  sinema  na  mwanaharakati  Angelina  Jolie alikuwa  mahakamani  hapo akisikiliza  hukumu  hiyo  na amesema  kuwa  hukumu  hiyo  ni ushindi  kwa  wanajeshi wa  zamani  watoto  ambao  wamekuwa  wakitumikia majeshi  ya  wababe  wa  kivita.

No comments:

Post a Comment