Na Steve Jonas
HALMASHAURI ya Jiji la Mbeya na Halmashauri ya Wilaya ya
Mbeya zimeingia kwenye mgogoro mkubwa wa ardhi baada ya Jiji kujiongezea eneo
katika Mlima Iwambi bila ya makubaliano na uongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya
Mbeya.
Habari zinasema kwamba,Halmashauri ya Jiji la Mbeya
limekiuka taratibu za mipaka ya ardhi inayo zitenganisha Halmashauri ya Wilaya
ya Mbeya na jiji kwa kupora eneo la ukubwa wa ekari 600 katika mlima maarufu
kwa jina la Iwambi.
Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbeya,Anderson
Kabenga ofisini kwake alisema kuwa jiji limepora ekari hizo ambazo ni ardhi ya
wananchi wake bila ya ridhaa yao kwa maelezo kuwa hakuna kikao walicho keti na
Halmashauri ya Jiji ili kumega eneo hilo kwaajili ya matumizi ya wananchi wa
Halmashauri ya Jiji.
Alisema kuwa sababu zinazo elezwa na uongozi wa Jiji zinadai
kwamba Jiji lilifanya hivyo kwa kusudi la kupanua Jiji kitendo ambacho Kabenga
alikitolea ufafanuzi kuwa kama ni upanuzi wa Jiji siyo tatizo lakini
zingefuatwa taratibu za kisheria kwa pande zote mbili kuketi pamoja na
kukubaliana kuhusu suala hilo.
Kabenga alisema kwamba,Halmashauri ya Wilaya ya Mbeya baada
ya kubaini uporwaji wa ardhi hiyo kiliitishwa kikao maaluma cha Baraza la
Madiwani wa Halmashauri hiyo ambacho kiliamua kuwatuma wajumbe wanne kwa Waziri
mwenye dhamana ili Waziri huyo afute tangazo Na237 la Desemba 12 mwaka 2005
lililotoka kwenye Gazeti la serikali.
Aidha ,alidokeza kuwa kusudi la Jiji kupora eneo hilo si
katika kupanua ukubwa wa Jiji pekee bali lililenga pia kupora vyanzo vya Mapato
kwa maelezo kuwa eneo hilo la ekari 600 lililopo katika mlima Iwambi lina
madini hivyo Jiji lilitaka kujipatia mapato kupitia eneo hilo ambalo ni eneo
halali la Halmashauri ya Wilaya ya Mbeya
Habari za uchunguzi na zinazo thibitisha kuwa eneo hilo lina
madini ,zimebaini kuwa kuna kampuni moja inayojihusisha na uchimbaji wa Madini
imewaandikia Barua wakazi wa eneo hilo inayo wataka wahame makazi yao lakini
wananchi wameweka mgomo kwani hawana taarifa za serikali sambamba na kufidiwa.
Hata hivyo,ofisi ya mkurugenzi wa Jiji haina taarifa za
wanachi kutakiwa wahame maeneo yao kwa maelezo kuwa hakuna mtu au kampuni inayo
miliki ardhi hiyo ambayo ni mali ya serikali.
No comments:
Post a Comment