Australia
imethibitisha hii leo kuwa ina inajiandaa juu ya uwezekano wa kumpeleka
Marekani raia wake Julian Assange.
Matayarisho hayo yanafanywa na
ubalozi wa nchi hiyo nchini Marekani ambao hata hivyo umesema kuwa ni mpango
utakaotegeme mambo mengine kadhaa. Waziri wa Biashara wa Australia Craig
Emerson amesema kuwa ubalozi huo mjini Washington unajiandaa na uwezekano wa
kumsalimisha Assange mikononi mwa Marekani na kusema kuwa jambo hilo ni kitu
cha kawaida kwenye masuala ya kidiplomasia. Katika mazungumzo yake na kituo cha
televisheni cha ABC, Emerson amesema kuwa ubalozi huo unatimiza wajibu wake wa
kuishauri serikali kama itaona kuna haja ya kumpeleka Assange nchini humo.
Taarifa hiyo inafuatia kuenea kwa ripoti kuwa ubalozi wa Australia mjini
Washington unahisi Marekani inamuwinda Assange. Assange alipewa
hifadhi katika ubalozi wa Equador jijini London mnamo mwezi Juni ili kukwepa
kusafirishwa kutoka Uingereza hadi Sweden kuhusiana na madai ya unyanyasaji
kingono. Mawaziri wa Mambo ya Kigeni kutoka Shirikisho la Mataifa ya Amerika
wanatarajiwa kukutana mjini Washington wiki ijayo kujadiliana kuhusu mgogoro
huo wa kidiplomasia.
No comments:
Post a Comment