Wednesday, August 15, 2012

WASTAAFU MBEYA WALALAMIKIA MALIPO YAO



WASTAAFU wa serikali mkoani Mbeya hivi karibuni wamelalamika juu ya ucheleweshwaji wa malipo yao ya pensheni ambayo kwa kawaida wanalipwa kila baada ya miezi mitatu.

Mmoja wa wastaafu hao aliyejitambulisha kwa jina la Martin Mwakalinga ,alisema kuwa kumekuwepo usumbufu wa kulipwa pensheni hizo tofauti na agizo la serikali linaloelezea wastaafu hao walipwe pesa za miezi mitatu kwa wakati mmoja.

Alisema kwamba,agizo hilo halijatekelezwa kwani kuna wakati wanalipwa malipo ya miezi miwili kwa wakati mmoja badala ya miezi mitatu huku akitolea mfano kuwa malipo ya mwezi julai 31 hadi Desemba mwaka jana hadi sasa hawajalipwa.

Aidha ,Mwakalinga ambaye alikuwa mtumishi katika idara ya Elimu na kustaafu mwaka 1996 alisema kuwa mbali ya tofauti hiyo pia malipo hayo hayalipwi kwa mtililiko  muafaka kitendo ambacho kinawaweka katika wakati mgumu na kushindwa kuazima pesa mahali kwingine kwaajili ya kujikimu.

‘Hatulipwi kwa wakati hali ambayo inatufanya tushindwe hata kukopa kwa watu pesa kwani hatuna uhakika ni wakati gain tutalipwa pensheni hizo,mfumo’Alisema na kuongeza kuwa mfumo uliopo umewaweka katika maisha ya kubahatisha.

Aliendelea kuitupia lawama serikali kwamba,imewapa kisogo kwa maelezo kuwa mnamo mwaka 2009 waliahidiwa kuongezewa malipo hayo ahadi ambayo alisema hadi sasa bado haijatekelezwa.

Sambamba na hayo ,mstaafu huyo aliomba serikali iwafikirie kwenye bajeti yake kuwaongezea wastaafu malipo hayo  wapate robo tatu ya mshahara wa kima cha chini kwa sasa ili kumudu maisha ya sasa ambayo alisema kuwa ni ghali kuliko miaka ya nyuma.

‘Tunaiomba serikali itufikirie kwenye bajeti ili kutupandishia malipo yetu kwa kuzingatia umuhimu wetu tulipokuwa tukilitumikia Taifa letu,tumesahaulika hata kujikuta kama hatukuwa na thamani katika utendaji wetu’.Alisema






No comments:

Post a Comment