Saturday, August 4, 2012

MKONGWE WA RIADHA AOMBA WADAU WA MCHEZO HUO KUJITOKEZA KUUPIGA TAFU



Mjumbe wa Kamati kuu ya Riadha Taifa na Katibu wa Kamati Riadha mkoa wa Mbeya Lwiza John amewataka wadau wa mchezo wa Riadha kujitokeza kuudhamini katika mkoa wa Mbeya kutoka na hali mbaya uliona nao mkoani humo.
Mwanariadha huyo amesema kuwa sasa mchezo wa Riadha katika mkoa wa Mbeya umepoteza mwelekeo kabisa kutokana na kuyumba kwa uchumi miongoni mwa jamii. 
Pia amesema inakuwa wakati mwingine ni ngumu kuwapata wachezaji wa mchezo huo  hususani wa kike kutokana na taifa kutoupa kipaumbele. Wiza ameongeza kusema changamoto wakiwa katika mchujo wa kupata wachezaji watakaokimbia katika Riadha Taifa inatokana na kukosa wadhamini kwani wachezaji wanakosa viatu, maji na vitu kama dawa hali inayokatisha tama kabisa wachezaji kujitokeza kwa wingi. Hata hivyo amewataka wachezaji kuwa na moyo mkuu kwa kuweza kuwa wazlendo na nchi yao licha ya chanagamoto zote wanazokutana nazo.

No comments:

Post a Comment